ADVERTISEMENT
SATURDAY, SEPTEMBER 29, 2012
FRANCIS CHEKA HANA MPINZANIA TANZANIA - AMDUNGA TENA KALAMA NYILAWILA
| Refarii wa mpambano akiwaelekeza mabondia wasicheze kwa kukumbatiana |
| Bondia Karama Nyilawila kulia akijitaidi kukwepa makonde ya mpinzani wake Fransic Cheka wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi cheka alishinda kwa K,o raundi ya sita. |
| Mabondia Karama Nyilawila kushoto akionesheana umwamba wa kutupa masumbwi na Fransic Cheka wakati wa mpambano wao cheka alishinda kwa K,O Raundi ya sitapicha nawww.superdboxingcoach. |
| Fransic Cheka kushoto na Karama Nyilawila wakiwa uringoni kuoneshana uwezo wa kutupiana masumbwi Cheka alishjnda kwa K,O ya Raundi ya sita picha na www.superdboxingcoach. |
| Mabondia Karama Nyilawila kushoto na Fransic Cheka wakionesheana umwamba wa kutupiana makonde wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Cheka alishinda kwa K,o raundi ya sita picha na www.superdboxingcoach. |
| Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach. |
| Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach. |
| Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach. |
--
SIMBA WALIVYOENDELEA KUNG'ARA LIGI KUU YA VODACOM DHIDI YA PRISONS
Mshambuliaji wa Simba, Felix Sunzu akiwatoka mabeki wa Tanzania Prisons
Wachezaji wa Simba wakishangilia bao la kwanza lililofungwa na Felix Sunzu (kulia)
Mashabiki wa Simba wakishangilia
Mshambuliaji wa Simba, mrisho Ngasa akichuana na nahodha wa Tanzania Prisons, Lugano Mwangama
Golikipa wa Prisons, David Abdallah akiokoa hatari langoni mwake
Wachezahi wa Prisons ya Mbeya wakiongozwa na kipa wao kuomba dua wakati wa mapumziko
![]() |
| Picha kwa hisani ya Habari Mseto |
LIVE MATCH CENTRE: SIMBA 2 - 1 TANZANIA PRISONS - FULL TIME
Amir Mafta anakula kadi nyekundu hapa kwa maana hiyo ataukosa mchezo dhidi ya Yanga.
DK 75: Simba bado wanaongoza katika kipindi hiki cha pili.
DK 68: Simba 2 - 1 Tanzania Prisons
DK 55: Mrisho anaingia kwenye box na kupiga shuti kali linalompita kipa wa Prisons na kutinga nyavuni na kuandikia Simba bao la pili.
Kipindi cha pili kimeanza kwa kasi sana, Mrisho Ngassa anaingia vizuri kwenye winga ya kulia, anapiga krosi safi na Sunzu anakosa bao la wazi.
Mpira ni mapumziko - Simba 1 - 1 Prisons
DK 45+1: Mrisho Ngassa anawapiga vyenga mabeki wa Prisons na kuachia shuti kali linalotoka nje kwa sentimita chache.
DK 45: Felix Sunzu anaipatia Simba bao la kusawazisha.
DK 35: Edward Christopher anaingia vizuri kwenye lango la Prisons, lakini anaingiliana na Sunzu na mabeki wa Prisons wanaokoa mpira langoni mwao.
DK 30: Simba wanalishambulia sana lango la Prisons wakitafuta bao la kusawazisha.
DK 20: Simba 0 - 1 Tanzania Prisons
DK 75: Simba bado wanaongoza katika kipindi hiki cha pili.
DK 68: Simba 2 - 1 Tanzania Prisons
DK 55: Mrisho anaingia kwenye box na kupiga shuti kali linalompita kipa wa Prisons na kutinga nyavuni na kuandikia Simba bao la pili.
Kipindi cha pili kimeanza kwa kasi sana, Mrisho Ngassa anaingia vizuri kwenye winga ya kulia, anapiga krosi safi na Sunzu anakosa bao la wazi.
Mpira ni mapumziko - Simba 1 - 1 Prisons
DK 45+1: Mrisho Ngassa anawapiga vyenga mabeki wa Prisons na kuachia shuti kali linalotoka nje kwa sentimita chache.
DK 45: Felix Sunzu anaipatia Simba bao la kusawazisha.
DK 35: Edward Christopher anaingia vizuri kwenye lango la Prisons, lakini anaingiliana na Sunzu na mabeki wa Prisons wanaokoa mpira langoni mwao.
DK 30: Simba wanalishambulia sana lango la Prisons wakitafuta bao la kusawazisha.
DK 20: Simba 0 - 1 Tanzania Prisons
SIMBA vs TANZANIA PRISONS LINE UPS
Timu za Simba na Tanzania Prisons zinapambana jioni hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni. Tayari makocha wa timu zote mbili Jumanne Charles (Tanzania Prisons) na Circo Milovan (Simba) wameshataja vikosi vyao.
Simba: Tanzania Prisons:
01.Juma Kaseja (c) 18.David Abdallah
02.Nassoro Masoud 03.Aziz Sibo
17.Amir Maftah 05.Laurian Mpalile
15.Shomari Kapombe 16.Lugano Mwangama (c)
24.Juma Nyoso 15.David Mwantika
14.Mwinyi Kazimoto 13.Khalid Fupi
28.Amri Kiemba 07.Misango Magai
08.Ramadhan Chombo 12.Fred Chudu
19.Edward Christopher 14.Elias Maguri
10.Felix Sunzu 17.Peter Michael
16.Mrisho Ngasa 19.John Matei
Wachezaji wa akiba;
22.Wilbert Mweta 01.Daudi Mwasongwe
23.Paul Ngalema 04.Jumanne Elfadhili
20.Jonas Mkude 09.Sino Augustino
12.Salim Kinje 22. Julius Kwaga
04.Komanbil Keita 08.Henry Mwalugala
13.Daniel Akuffor 11.Hamisi Ally
05.Pascal Ochieng 23.Jeremiah Juma
Refa: Paul Soleji (Mwanza)
Mwamuzi Msaidizi 1: Jesse Erasmo (Morogoro)
Mwamuzi Msaidizi 2: Mwarabu Mumba (Morogoro)
Mwamuzi wa Akiba: Israel Nkongo (Dar es Salaam
HIVI NDIO VIINGILIO VYA MECHI YA SIMBA NA YANGA
KIINGILIO MECHI YA YANGA, SIMBA SH. 5,000
Kiingilio cha chini kwenye mechi ya Yanga na Simba itakayochezwa Jumatatu (Oktoba 3 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648 kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000.
Mechi hiyo namba 80 ya Ligi Kuu ya Vodacom itachezwa kwenye uwanja huo kuanzia saa 11 kamili jioni. Watazamaji watakaotaka kuona mechi hiyo wakiwa wameketi kwenye viti vya rangi ya bluu ambavyo ni 17,045 watalipa sh. 7,000 kwa tiketi moja.
HUYU NDIO KOCHA MPYA WA YANGA - ERNIE BRANDTS
Hatimaye leo hii klabu bingwa ya Afrika mashariki na kati Dar Young Africans imemtambulisha rasmi kocha wake mpya Mholanzi Ernie Brandts.
Kocha huyu ambaye miezi michache iliyopita alikuwa mwalimu wa klabu bingwa ya Rwanda, APR aliwasili jijini Dar es Salaam jana usiku na leo asubuhi ametambulishwa rasmi kwa waandishi wa habari na kusaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuifundisha klabu hiyo ya Jangwani.
Brandts ambaye amewahi kuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Uholanzi na klabu kubwa ya nchi hiyo PSV Eindhoven akicheza kwenye nafasi ya ulinzi, amekuja Yanga kuchukua nafasi ya mbelgiji Tom Saintfiest aliyetimuliwa wiki iliyopita baada ya kukaa kwenye klabu hiyo kwa siku 81.
HII NDIO PROFILE YA KOCHA MPYA WA YANGA ERNIE BRANDT.
| Personal information | |||
|---|---|---|---|
| Full name | Ernstus Wilhelmus Johannes Brandts | ||
| Date of birth | 3 February 1956 (age 56) | ||
| Place of birth | Nieuw-Dijk, Gelderland | ||
| Height | 1.81 m (5 ft 11 1⁄2 in) | ||
| Playing position | Defender (retired) | ||
| Club information | |||
| Current club | APR FC | ||
| Youth career | |||
| De Sprinkhanen (Nieuw-Dijk) | |||
| Senior career* | |||
| Years | Team | Apps† | (Gls)† |
| 1974–1977 | De Graafschap | 38 | (2) |
| 1977–1986 | PSV Eindhoven | 251 | (23) |
| 1986–1989 | Roda JC | 68 | (4) |
| 1988–1989 | MVV Maastricht | 16 | (0) |
| 1989–1991 | K.F.C. Germinal Beerschot | 59 | (5) |
| 1991–1992 | De Graafschap | 20 | (0) |
| National team | |||
| 1977–1985 | Netherlands | 28 | (5) |
| Teams managed | |||
| 1993–2002 | PSV Eindhoven (youth and assistant) | ||
| 2002–2004 | RKSV Nuenen | ||
| 2005–2006 | FC Volendam | ||
| 2006–2008 | NAC Breda | ||
| 2009 | Rah Ahan | ||
| 2010– | APR FC | ||
FRIDAY, SEPTEMBER 28, 2012
KWANINI CRISTIANO RONALDO NI TIGER WOODS WA SOKA
Cristiano Ronaldo ni mmoja ya wachezaji bora kabisa wa juu katika kizazi hiki. Jinsi alivyoitawala La Liga katika misimu miwili inatukumbusha mmoja wa wanamichezo bora kabisa katika karne hiii: Tiger Woods.
Pamoja na kwamba wanacheza kwenye michezo miwili tofauti, wawili hawa wana vitu vingi wanavyofanana. Wote wawili ni wachezaji muhimu sana katika michezo yao na wamaekuwa ni wenye mafanikio. Wameweza kupata madili mengi ya udhamini na huku wakicheza kwenye kiwango cha kuvunja rekodi.
Tiger na CR7 wamejituma sana mpaka kufikia malengo yao: wakicheza kwa kiwango cha juu ili kuwa wachezaji bora kabisa kwenye michezo yao husika.
Wawili hawa wanafanana katika vitu na hivi vifuatavyo ni baadhi.
MAPATO
Kwa mujibu wa Forbes, Tiger Woods ni mwanamichezo wa tatu anayelipwa vizuri zaidi duniani. Mshahara pekee unafikia kiasi cha $4.4 million kwa mwaka.
Cristiano Ronaldo pia yupo katika listi hiyo, akishika nafasi ya 9. Ingawa David Beckham anaongoza kwa mapato ya jumla, lakini mshahara wa Cristiano Ronaldo kwa mwaka upo karibia na $20.5 million, jambo ambalo linamaanisha anamzidi $11.5 million Beckham.
Hii inawafanya kuwa wanamichezo wenye kulipwa vizuri zaidi kwenye michezo yao - bila kuingiza mapato ya udhamini.
KUPENDWA NA KUCHUKIWA
Wanamichezo hawa wawili wana fan base kubwa sana na pia wanachukia sana. Kwa Tiger mambo yote yalianza ilipotoka skendo yake ya kumsaliti mkewe mwaka 2009. Taswira yake ya kuwa mume bora ikafutika na kuchukiwa na watu wengi.
Cristiano yeye na mwenzake Lionel Messi wamewagawa wapenzi wa mpira wa miguu duniani. Pia tabia zake za nje ya uwanja zimezidi kumuongezea maadui, muda mwingine tambo zake tu zimekuwa zikimfanya watu wamchukie.
Kwa wale wanaowapenda hakuna kitu kingine wanachojali zaidi ya ushujaa wao.
KIWANGO
Tiger ni mmoja kati ya wacheza gofu bora kabisa kuwahi kutokea duniani. Wengi wanamuona kama ni bora zaidi ya Jack Nickalus, wengine wanaamini kwamba hatoweza kumshinda Jack mpaka pale atakaposhinda makombe makubwa zaidi ya 18.
Cristiano amekuwa nae akihusishwa na mjadala kama huo, lakini kwa mara nyingi zaidi amekuwa akifananishwa na Lionel Messi. Mwaka 2008 alishinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia na amekuwa akiendelea kutisha tangu wakati huo.
Wote wamekuwa kwenye viwango vya juu kwa miaka mingi, kwa Woods kipindi chake kizuri kabisa kilikuwa mwaka 2000.
Alishinda makombe sita mfululizo, kitu ambacho hakuna yoyote aliyeweza tangu mwaka 1948, alishinda katika michuano ya US Open,, kitu ambacho Sports Illustrated walisema kiwango cha Woods kwenye michuano hiyo kilikuwa bora kuliko vyote katika historia ya gofu.
Katika misimu 16 kama mcheza gofu, Tiger ameshinda katika michuano 102, 74 kati ya hiyo ameshinda katika PGA Tour.
Ronaldo amekuwa akicheza soka la ushindani wa juu kwa miaka 10 sasa ambayo amefanikiwa kufunga mabao 275 na Sporting Lisbon, Manchester United na Real Madrid, na mabao mengine 37 katika timu ya taifa ya Ureno, jumla ya mabao yote ni 312.
CR7 aliwakusanya mashabiki 85,000 katika utambulishwaji wake pale Bernabeu, akivunja rekodi ya Maradona ya kutambulishwa mbele ya mashabiki 75,000 alipoiunga na Napoli.
Alihitaji mechi nne kuweka historia na Los Blancos, alifunga katika kila mechi zake nne za mwanzo, akiwa ndio mchezaji wa kwanza kufanya hivyo.
Moja ya mafanikio yake makubwa hivi karibuni aliweza kumaliza msimu wa La liga akiwa amefunga mabao 40, kitu ambacho hakuna aliyewahi kufanya hivyo; Hugo Sanchez na Telmo Zarra walikuwa wamefunga mabao 38 kila mmoja huko nyuma.
MITANDAO YA KIJAMII
Tiger Woods ndi mcheza gofu mwenye mashabiki wengi kwenye mtandao wa Twitter.
Alipofungua akaunti yake akuwa akitweet sana, lakini baada ya skendo ya kuisaliti ndoa yake, akaanza kuitumia akaunti yake.
Cristiano Ronaldo nae ana sifa hiyo hiyo ya Woods, lakini pia ameweza kuwa mwanamichezo mwenye mashabiki wengi zaidi kwenye mtandao huo akiwa na followers zaidi ya millioni 13.
MIKATABA YA UDHAMINI
Nike, NetJets, EA Sports, Konami, Rolex, na wengine kibao. Wote wanawadhamini hawa vijana. Wachezaji hawa wawili hawa wana wadhamini bora kabisa kwenye michezo.
Woods anatengezea kiasi cha $55 million kwa mwaka kutokana na mapato ya mikataba ya matangazo. Mchezaji huyo bora namba 1 wa zamani aliwapoteza wadhamini kama Gatorade, AT&T, Buick na Tag Heur katika miaka kadhaa iliyopita, lakini ndio mwanamichezo anayeokea fedha nyingi kutoka mikataba ya matangazo.
Katika upande wa Ronaldo anashika nafasi ya 10 na wa pili nyuma ya David Beckham kama mwanasoka mwenye mapato makubwa kutokana na mikataba ya matangazo ya biashara.
Pamoja na kwamba wanacheza kwenye michezo miwili tofauti, wawili hawa wana vitu vingi wanavyofanana. Wote wawili ni wachezaji muhimu sana katika michezo yao na wamaekuwa ni wenye mafanikio. Wameweza kupata madili mengi ya udhamini na huku wakicheza kwenye kiwango cha kuvunja rekodi.
Tiger na CR7 wamejituma sana mpaka kufikia malengo yao: wakicheza kwa kiwango cha juu ili kuwa wachezaji bora kabisa kwenye michezo yao husika.
Wawili hawa wanafanana katika vitu na hivi vifuatavyo ni baadhi.
MAPATO
Kwa mujibu wa Forbes, Tiger Woods ni mwanamichezo wa tatu anayelipwa vizuri zaidi duniani. Mshahara pekee unafikia kiasi cha $4.4 million kwa mwaka.
Cristiano Ronaldo pia yupo katika listi hiyo, akishika nafasi ya 9. Ingawa David Beckham anaongoza kwa mapato ya jumla, lakini mshahara wa Cristiano Ronaldo kwa mwaka upo karibia na $20.5 million, jambo ambalo linamaanisha anamzidi $11.5 million Beckham.
Hii inawafanya kuwa wanamichezo wenye kulipwa vizuri zaidi kwenye michezo yao - bila kuingiza mapato ya udhamini.
KUPENDWA NA KUCHUKIWA
Wanamichezo hawa wawili wana fan base kubwa sana na pia wanachukia sana. Kwa Tiger mambo yote yalianza ilipotoka skendo yake ya kumsaliti mkewe mwaka 2009. Taswira yake ya kuwa mume bora ikafutika na kuchukiwa na watu wengi.
Cristiano yeye na mwenzake Lionel Messi wamewagawa wapenzi wa mpira wa miguu duniani. Pia tabia zake za nje ya uwanja zimezidi kumuongezea maadui, muda mwingine tambo zake tu zimekuwa zikimfanya watu wamchukie.
Kwa wale wanaowapenda hakuna kitu kingine wanachojali zaidi ya ushujaa wao.
KIWANGO
Tiger ni mmoja kati ya wacheza gofu bora kabisa kuwahi kutokea duniani. Wengi wanamuona kama ni bora zaidi ya Jack Nickalus, wengine wanaamini kwamba hatoweza kumshinda Jack mpaka pale atakaposhinda makombe makubwa zaidi ya 18.
Cristiano amekuwa nae akihusishwa na mjadala kama huo, lakini kwa mara nyingi zaidi amekuwa akifananishwa na Lionel Messi. Mwaka 2008 alishinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia na amekuwa akiendelea kutisha tangu wakati huo.
Wote wamekuwa kwenye viwango vya juu kwa miaka mingi, kwa Woods kipindi chake kizuri kabisa kilikuwa mwaka 2000.
Alishinda makombe sita mfululizo, kitu ambacho hakuna yoyote aliyeweza tangu mwaka 1948, alishinda katika michuano ya US Open,, kitu ambacho Sports Illustrated walisema kiwango cha Woods kwenye michuano hiyo kilikuwa bora kuliko vyote katika historia ya gofu.
Katika misimu 16 kama mcheza gofu, Tiger ameshinda katika michuano 102, 74 kati ya hiyo ameshinda katika PGA Tour.
Ronaldo amekuwa akicheza soka la ushindani wa juu kwa miaka 10 sasa ambayo amefanikiwa kufunga mabao 275 na Sporting Lisbon, Manchester United na Real Madrid, na mabao mengine 37 katika timu ya taifa ya Ureno, jumla ya mabao yote ni 312.
CR7 aliwakusanya mashabiki 85,000 katika utambulishwaji wake pale Bernabeu, akivunja rekodi ya Maradona ya kutambulishwa mbele ya mashabiki 75,000 alipoiunga na Napoli.
Alihitaji mechi nne kuweka historia na Los Blancos, alifunga katika kila mechi zake nne za mwanzo, akiwa ndio mchezaji wa kwanza kufanya hivyo.
Moja ya mafanikio yake makubwa hivi karibuni aliweza kumaliza msimu wa La liga akiwa amefunga mabao 40, kitu ambacho hakuna aliyewahi kufanya hivyo; Hugo Sanchez na Telmo Zarra walikuwa wamefunga mabao 38 kila mmoja huko nyuma.
MITANDAO YA KIJAMII
Tiger Woods ndi mcheza gofu mwenye mashabiki wengi kwenye mtandao wa Twitter.
Alipofungua akaunti yake akuwa akitweet sana, lakini baada ya skendo ya kuisaliti ndoa yake, akaanza kuitumia akaunti yake.
Cristiano Ronaldo nae ana sifa hiyo hiyo ya Woods, lakini pia ameweza kuwa mwanamichezo mwenye mashabiki wengi zaidi kwenye mtandao huo akiwa na followers zaidi ya millioni 13.
MIKATABA YA UDHAMINI
Nike, NetJets, EA Sports, Konami, Rolex, na wengine kibao. Wote wanawadhamini hawa vijana. Wachezaji hawa wawili hawa wana wadhamini bora kabisa kwenye michezo.
Woods anatengezea kiasi cha $55 million kwa mwaka kutokana na mapato ya mikataba ya matangazo. Mchezaji huyo bora namba 1 wa zamani aliwapoteza wadhamini kama Gatorade, AT&T, Buick na Tag Heur katika miaka kadhaa iliyopita, lakini ndio mwanamichezo anayeokea fedha nyingi kutoka mikataba ya matangazo.
Katika upande wa Ronaldo anashika nafasi ya 10 na wa pili nyuma ya David Beckham kama mwanasoka mwenye mapato makubwa kutokana na mikataba ya matangazo ya biashara.
SIMBA MPENI NAFASI HUYU KINDA: ANAWEZA KUZIBA PENGO LA OKWI DHIDI YA YANGA
Wakati joto la pambano la kwanza la ligi la watani wa jadi Simba na Yanga likizidi kupamba moto, huku Simba wakiwa na pengo kubwa la kumkosa mshambuliaji wao tegemeo Emmanuel Okwi ambaye ana adhabu ya kufungiwa mechi tatu - mashabiki na wanachama wa klabu hiyo pamoja na benchi la ufundi la Simba hawapaswi kuwa fikra kubwa kuhusu pengo la Okwi.
Bahati nzuri ni kwamba Simba walijitahidi kufanya usajili mzuri kwenye safu ya ushambuliaji msimu huu hivyo wapo baadhi ya wachezaji ambao wanaweza kucheza vizuri na kuziba pengo la Okwi. Mmoja ya wachezaji hao ni kinda huyu aliyepandishwa kutoka Simba B iliyochukua ubingwa wa BancABC Super8 anayeitwa Haruni Athumani Chanongo.
Kijana huyu mwenye miaka 20, alikuwa ni mmoja ya wachezaji waliong'ara vilivyo katika michuano hiyo ya Super8, akizisumbua vilivyo ngome za vilabu vya ligi kuu vya Azam na Mtibwa katika mechi za nusu fainali na fainali huku akiwa mmoja ya wafungaji wazuri.
Staili ya uchezaji ya kinda huyu haitofautiani sana na ya Okwi, ana kasi na ujuzi wa kupiga vyenga. Anajiamini na ana uwezo wa kupambana katika kuisadia Simba kipindi hiki ikiwa na pengo la mshambuliaji tegemeo Okwi.
Haruni ambaye mwanzoni alishawahi kuichezea Polisi Dodoma katika ligi kuu chini kocha Sekilojo Chambua, tayari ana uzoefu wa kucheza mechi kubwa na kupafomu vizuri. Hapa anaelezea:
"Nilipokuwa na umri wa miaka 18 nikiwa na timu ya Polisi Dodoma,kocha Sekilojo Chambua alinipa nafasi ya kucheza mchezo wangu wa kwanza wa ligi kuu ya Vodacom. Nafasi hii ilitokea baada ya baadhi ya wachezaji wa kikosi cha kwanza kuondoka kutokana na timu kuwa na matokeo mabaya,mchezo wangu wa kwanza ulikua dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Jamhuri uliomalizika kwa sare ya bao 1:1.
Nikiwa na Polisi pia nilifanikiwa kucheza michezo dhidi ya Simba na Yanga iliyomalizika kwa timu yetu kufungwa mechi zote mbili mabao 2:0."
Kwa mujibu wa makocha ambao tayari wameshamfundisha kinda huyu wanasema Haruni ana uwezo mkubwa na anaweza kucheza vizuri kwenye yoyote kwa sababu ana uwezo na anajiamini.
Kwa mujibu wa makocha ambao tayari wameshamfundisha kinda huyu wanasema Haruni ana uwezo mkubwa na anaweza kucheza vizuri kwenye yoyote kwa sababu ana uwezo na anajiamini.
DERRICK WALULYA, TONY NDOLO, NA ERNEST BOAKYE WAOMBEWA UHAMISHO WA KIMATAIFA
TFF YATOA ITC KWA WACHEZAJI WANNE
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa wachezaji wanne waliokuwa wakichezea timu mbalimbali nchini.
Wachezaji hao ni Tony Ndolo aliyejiunga na KCC ya Uganda kutoka Toto Africans, Felix Amech Stanley aliyekwenda Bahla ya Oman kutoka Coastal Union, Ernest Boakye kutoka Yanga aliyejiunga na Tripoli Athletics Club ya Lebanon na Derrick Walulya aliyerejea URA ya Uganda kutoka Simba.
15 WACHUKUA FOMU UCHAGUZI TWFA
Wanamichezo 15 wamechukua fomu kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) utakaofanyika mwanzoni mwa mwezi ujao.
Waliochukua fomu za kuwania uenyekiti ni Lina Kessy, Isabellah Kapera na Joan Minja. Nafasi ya Makamu Mwenyekiti imeombwa na Roseleen Kisiwa pekee wakati Katibu Mkuu ni Amina Karuma na Cecilia Makafu. Macky Mhango pia ni mwombaji pekee aliyeomba nafasi ya Katibu Msaidizi.
Waombaji watatu wa nafasi ya mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ni Furaha Francis, Juliet Mndeme na Zena Chande. Nafasi ya Mhazini nayo ina mwombaji mmoja tu ambaye ni Rose Msamila.
Sophia Charles, Rahim Maguza, Telephonia Temba na Jasmin Badar Soud wao wanaomba nafasi ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya chama hicho kwenye uchaguzi huo ambao utaendeshwa na Kamati ya Uchaguzi ya TWFA chini ya Ombeni Zavalla.
MKUTANO VODACOM, KLABU ZA LIGI KUU
Klabu za Ligi Kuu na mdhamini wa ligi hiyo kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom zimekutana jana (Septemba 27 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
Mazungumzo yalilenga kipengele ya upekee (exclusivity) kilichopo kwenye mkataba wa udhamini ambacho kitaendelea kuwepo. Klabu zilikuwa zimeomba kwa mdhamini kuangalia uwezekano wa kukiondoa.
Pande hizo zimekubaliana kuunda kamati ya pamoja kwa ajili ya kuitafutia kila klabu mdhamini binafsi kwa lengo la kuhakikisha zinashiriki kikamilifu katika ligi hiyo.
Klabu zote zimeshapata vifaa kutoka kwa Vodacom ukiondoa African Lyon ambayo ilitarajia kuchukua vifaa hivyo leo kutoka kwa mdhamini wa ligi hiyo.
MCHAKATO WA UCHAGUZI WA VIONGOZI TAFCA
Mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) unaanza rasmi Septemba 30 mwaka huu kwa uchukuaji fomu kwa wagombea.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TAFCA, Ramadhan Mambosasa, fomu kwa waombaji uongozi zitaanza kutolewa Septemba 30 mwaka huu, na mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu hizo ni Oktoba 4 mwaka huu.
Fomu hizo zinapatikana ofisi za TAFCA zilizopo Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 alasiri. Ada ya fomu kwa waombaji wa nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu na Katibu Msaidizi ni sh. 200,000.
Nafasi zilizobaki za Mhazini, mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na wajumbe wa Kamati ya Utendaji, ada ya fomu ni sh. 100,000. Uchaguzi wa TAFCA umepangwa kufanyika Novemba 10 mwaka huu.
MCHEZO WA MASUMBWI, TAA INAYOZIZIMA – SEHEMU YA PILI
■UNAPENDWA NA KUOGOPWA NA WATU WENGI DUNIANI
■UKO HATARINI KUPOTEZA ASILI YAKE KABISA
Na Onesmo Ngowi
Masumbiwi au kwa majina mwengine ndondi au ngumi na kwa majina ya mitaani ndogwa, mawe n.k. ni mchezo unapoendwa sana na watu wengi. Aidha mchezo huu ni kati ya michezo inayoogopwa sana duniani. Mchezo wa ngumi uko hatarini kupoteza maana yake ya asili yaani kucheza kama burudani, kuwakilisha nchi na kujenga ushupavu wa mchezaji. Mamilioni ya watu wanaojazana kuutazama wasingependa kabisa kujiingiza kuucheza mchezo wa ngumi. Sasa endelea………………………………….! Kuanzia karne ya 16 matukio mbalimbali yaliyotokea katika bara la Ulaya na Mashariki ya mbali yalichochea ustaarabu uliopelekea mambo mengi kubadilika. Mabadiliko haya ni pamoja na watu walivyokuwa wanachukuliwa na kuthaminiwa.
2) Awe ni mtu anayeishi maisha yasiyo na kasheshe
3) Awe ni mtu aliyefikia kiwango cha juu katika fani yake na kuitetea bila ya matatizo.
4)Na zaidi ya yote awe mtu anayependa nchi yake na kuitetea katika fani yake bila kujali faida anayoweza kuipata.
THURSDAY, SEPTEMBER 27, 2012
TFF,FA MIKOA NA NMB MNATUPELEKA WAPI ?
Habari zenu ndugu wasomaji. Leo nina maswali machache na hoja kadhaa ambazo nahitaji majibu toka kwa TFF, FA MIKOA na Benki ya NMB kama wadau wakubwa wa Soka hapa nchini.
Naamini kila mtu anakumbuka kozi za Walimu wa Soka zilizokuwa zinafanyika hapa nchini takiribani mikoa yote ya Tanzania na baadhi ya mikoa ilijirudia mara kadhaa, Na nyingi ziliendeshwa kwa Walimu wa Sekondari na Shule za msingi ili kuinua vipaji toka mashuleni, hii inatokana na TFF kuangahika kwa muda mrefu kutafuta Wadhamini na hatimaye Benki ya NMB kujitokeza na kudhamini kozi hizi kitu ambacho ni kizuri kinachohitajika katika kukuza Soka letu Tanzania.
Kilichonishtua ni mwaka 2009/2010 ilitakiwa kuendeshwa kozi hiyo kwa mikoa 26 ya Tanzania Bara na Benki ya NMB ilitoa fedha za kuendesha kozi hiyo pamoja na mipira 30 kila mkoa,koni 18 kila mkoa, jezi jozi moja kwa ajili ya mkufunzi na fedha walipewa TFF ili watume kwa kila FA mkoa kwa mikoa yote 26.
Lakini cha kushangaza hawa TFF walituma pesa hizi na vifaa hivyo kwa mikoa kama kumi tu ikiwamo Shinyanga, Mwanza, Singida, mikoa ya Kisoka Ilala,Temeke na Kinondoni na pia fedha Tshs 710,000 kwa ajili ya posho ya mkufunzi, chakula, malazi na mawasiliano sasa swali je fedha nyingine za mikoa 16 zimekwenda wapi mimi na wewe msomaji wangu hatujui.
FA za mikoa teule ambayo ilipewa fedha hizo pia nao walichakachua kwa mtindo wao na kutoa fedha hizo kwa ufinyo Mfano ni Mkoa wa Shinyanga ambao kozi iliendeshwa januari 26, 2010-Februari 7,210 na mkufunzi alikuwa Marehemu Suleiman Gwaje ambaye pia alilalamikia hili, pia ulitokea ugomvi na kurushiana maneno kati ya viongozi wa FA mkoa na Wajumbe Watendaji kutokana na fedha hizo mpaka baadhi ya wajumbe kutaka kupindua uongozi huliopo madarakani.
Utaratibu ulitakiwa kuwa hivi mkufunzi akabidhiwe fedha zake katika mchanganuo ufuatao: - Posho ya siku 16 @ Tshs30, 000 jumla 480, 000, Nauli Tshs 230,000 yaani kwenda na kurudi pamoja na mawasiliano akiwa katika kituo chake cha kazi. Matokeo yake haya hayakufanyika na mkufunzi alipelekwa katika migahawa ya ajabu yenye bei nafuu na huduma hisiolidhisha ili kupiga panga fedha hizo.
Wanafunzi waliotakiwa kushiliki kozi hizi walikuwa ni Walimu na idadi ni 45 kwa kila mkoa yaani katika ile mikoa 10 teule ya TFF. Kwa mjibu wa TFF wenyewe walisema gharama ya Cheti kimoja ni Tshs 10,000 na fedha hizi ulipwa na NMB na tayari zilishakabidhiwa kwa TFF lakini cha kushangaza hakuna hata mkoa moja kati ya mikoa hii 10 walioendesha kozi hii mwaka 2009/2010 wamepata Vyeti hivyo. Sasa piga hesebu mikoa 26, kila mkoa Walimu 45 na kila mmoja gharama ya cheti ndio hiyo je ni Shilingi ngapi zimechakachuliwa na hawa jamaa?
Kinachoendelea sasa kuna kampeni ya TFF ya chini kwa chini kuhamasisha makatibu wa TAFCA wa ile mikoa ambayo ilibahatika kufanya kozi hii kuwaomba Walimu walioshiriki kozi hii wachange elfu kumi (Tshs 10,000) ili watengenezewe Vyeti hivyo kwa kupitia kwa Katibu wa TAFCA Taifa ili kuficha hili lilofanyika ambalo pia limekwama kutokana na kutokuwa na imani tena na TFF, sasa mimi najiuliza Soka letu litakua kwa mtindo huu? TFF, FA MIKOA na Benki ya NMB wanatupeleka wapi?
Pia baadhi ya mikoa kozi hii ilifanyika mwezi Oktoba 2009 kama Singida, Mwanza na mingineyo lakini Shinyanga ilifanyika tarehe 26 Januari, 2010 pia badala ya kuwa na Walimu 45 wa sekondari na shule za msingi waliotakiwa kushiriki walishiriki 26 tu tena katika mazingira magumu kwani hapakuwa na hata maji ya kunywa na washiriki walio wengi walifanya kuwakamata tu barabarani na kuwataka washiriki kozi hii na hili lilifanywa makusudi kwani fedha ya kuendesha kozi hii kwa mkoa huu ilikuwa ishaliwa na viongozi wa FA mkoa.
Na maelezo kutoka TFF, washiriki walitakiwa kujigharamia chakula na malazi kitu ambacho walikifanya Walimu hawa tena bila kinyongo. Je ni kweli ndio mkataba unavyosema maana mkataba huu ni siri kati ya TFF na Benki ya NMB hakuna mdau wala TAFCA anayeufahamu mkataba huo sasa tujiulize watu wakikataa kujitokeza kushiriki kozi hizi tutamlaumu nani kwa ubabahishaji huu?
Na kwa nini fedha hizi zisikabidhiwe kwa chama cha makocha Taifa na kuwambia waendeshe kozi hizi badala ya FA za kila mkoa kwani wao ndo wanajua watu gani ambao wanapenda na wanataka kuwa walimu wa soka.
Mimi kama mimi siamini kama Benki ya NMB hailifahamu hili kwani kama hawafahamu inaamana hawafanyi ukaguzi wa fedha zao wanazotoa kwa TFF? Na kama wanafahamu wamechukua hatua gani? Na kama wamechukua mbona taarifa hatujaiona wala kuisikia? Kama hawajachukua hatua inamaana na wao pia wanahusika katika hili?
Mimi kama mdau wa Soka hili la Bongo inaniuma sana na kubakia na maswali TFF, FA MIKOA na Benki ya NMB wanatupeleka wapi? Na wapo kwa ajili ya kuendeleza Soka au maslahi yao binafsi? TFF Na Benki ya NMB naomba mchunguze au mtoe maelezo kuhusu hili maana linatia kinyaa na aibu katika Soka letu na kama hamna taarifa basi Habari ndiyo hiyo.
Na Magesa Japhari
E – Mail: japharimagesa@yahoo.com
Mobile phone: +255 784 269 812 or +255 764 318 844, +255 714 368 843.
NB:
Kwa haraka haraka tu, Fedha inayosadikika kutafunwa na TFF na FA MIKOA
Watu 45 @ mkoa × 10,000 gharama ya cheti × 26 mikoa iliyotakiwa kushiriki jumla 11,700,000.
FEDHA ya Wakufunzi mikoa 26,ilitolewa kwa mikoa 10, je mikoa 16@Tshs 710,000 × 16 mikoa ambayo haikutumiwa jumla 11,360,000
GRAND TOTAL Tshs 23,060,000
Hizi ndizo tulizojua kwa mjibu wa hesebu iliyopo je tusizozifahamu ni ngapi? AKILI KUMKICHWA!
Naamini kila mtu anakumbuka kozi za Walimu wa Soka zilizokuwa zinafanyika hapa nchini takiribani mikoa yote ya Tanzania na baadhi ya mikoa ilijirudia mara kadhaa, Na nyingi ziliendeshwa kwa Walimu wa Sekondari na Shule za msingi ili kuinua vipaji toka mashuleni, hii inatokana na TFF kuangahika kwa muda mrefu kutafuta Wadhamini na hatimaye Benki ya NMB kujitokeza na kudhamini kozi hizi kitu ambacho ni kizuri kinachohitajika katika kukuza Soka letu Tanzania.
Kilichonishtua ni mwaka 2009/2010 ilitakiwa kuendeshwa kozi hiyo kwa mikoa 26 ya Tanzania Bara na Benki ya NMB ilitoa fedha za kuendesha kozi hiyo pamoja na mipira 30 kila mkoa,koni 18 kila mkoa, jezi jozi moja kwa ajili ya mkufunzi na fedha walipewa TFF ili watume kwa kila FA mkoa kwa mikoa yote 26.
Lakini cha kushangaza hawa TFF walituma pesa hizi na vifaa hivyo kwa mikoa kama kumi tu ikiwamo Shinyanga, Mwanza, Singida, mikoa ya Kisoka Ilala,Temeke na Kinondoni na pia fedha Tshs 710,000 kwa ajili ya posho ya mkufunzi, chakula, malazi na mawasiliano sasa swali je fedha nyingine za mikoa 16 zimekwenda wapi mimi na wewe msomaji wangu hatujui.
FA za mikoa teule ambayo ilipewa fedha hizo pia nao walichakachua kwa mtindo wao na kutoa fedha hizo kwa ufinyo Mfano ni Mkoa wa Shinyanga ambao kozi iliendeshwa januari 26, 2010-Februari 7,210 na mkufunzi alikuwa Marehemu Suleiman Gwaje ambaye pia alilalamikia hili, pia ulitokea ugomvi na kurushiana maneno kati ya viongozi wa FA mkoa na Wajumbe Watendaji kutokana na fedha hizo mpaka baadhi ya wajumbe kutaka kupindua uongozi huliopo madarakani.
Utaratibu ulitakiwa kuwa hivi mkufunzi akabidhiwe fedha zake katika mchanganuo ufuatao: - Posho ya siku 16 @ Tshs30, 000 jumla 480, 000, Nauli Tshs 230,000 yaani kwenda na kurudi pamoja na mawasiliano akiwa katika kituo chake cha kazi. Matokeo yake haya hayakufanyika na mkufunzi alipelekwa katika migahawa ya ajabu yenye bei nafuu na huduma hisiolidhisha ili kupiga panga fedha hizo.
Wanafunzi waliotakiwa kushiliki kozi hizi walikuwa ni Walimu na idadi ni 45 kwa kila mkoa yaani katika ile mikoa 10 teule ya TFF. Kwa mjibu wa TFF wenyewe walisema gharama ya Cheti kimoja ni Tshs 10,000 na fedha hizi ulipwa na NMB na tayari zilishakabidhiwa kwa TFF lakini cha kushangaza hakuna hata mkoa moja kati ya mikoa hii 10 walioendesha kozi hii mwaka 2009/2010 wamepata Vyeti hivyo. Sasa piga hesebu mikoa 26, kila mkoa Walimu 45 na kila mmoja gharama ya cheti ndio hiyo je ni Shilingi ngapi zimechakachuliwa na hawa jamaa?
Kinachoendelea sasa kuna kampeni ya TFF ya chini kwa chini kuhamasisha makatibu wa TAFCA wa ile mikoa ambayo ilibahatika kufanya kozi hii kuwaomba Walimu walioshiriki kozi hii wachange elfu kumi (Tshs 10,000) ili watengenezewe Vyeti hivyo kwa kupitia kwa Katibu wa TAFCA Taifa ili kuficha hili lilofanyika ambalo pia limekwama kutokana na kutokuwa na imani tena na TFF, sasa mimi najiuliza Soka letu litakua kwa mtindo huu? TFF, FA MIKOA na Benki ya NMB wanatupeleka wapi?
Pia baadhi ya mikoa kozi hii ilifanyika mwezi Oktoba 2009 kama Singida, Mwanza na mingineyo lakini Shinyanga ilifanyika tarehe 26 Januari, 2010 pia badala ya kuwa na Walimu 45 wa sekondari na shule za msingi waliotakiwa kushiriki walishiriki 26 tu tena katika mazingira magumu kwani hapakuwa na hata maji ya kunywa na washiriki walio wengi walifanya kuwakamata tu barabarani na kuwataka washiriki kozi hii na hili lilifanywa makusudi kwani fedha ya kuendesha kozi hii kwa mkoa huu ilikuwa ishaliwa na viongozi wa FA mkoa.
Na maelezo kutoka TFF, washiriki walitakiwa kujigharamia chakula na malazi kitu ambacho walikifanya Walimu hawa tena bila kinyongo. Je ni kweli ndio mkataba unavyosema maana mkataba huu ni siri kati ya TFF na Benki ya NMB hakuna mdau wala TAFCA anayeufahamu mkataba huo sasa tujiulize watu wakikataa kujitokeza kushiriki kozi hizi tutamlaumu nani kwa ubabahishaji huu?
Na kwa nini fedha hizi zisikabidhiwe kwa chama cha makocha Taifa na kuwambia waendeshe kozi hizi badala ya FA za kila mkoa kwani wao ndo wanajua watu gani ambao wanapenda na wanataka kuwa walimu wa soka.
Mimi kama mimi siamini kama Benki ya NMB hailifahamu hili kwani kama hawafahamu inaamana hawafanyi ukaguzi wa fedha zao wanazotoa kwa TFF? Na kama wanafahamu wamechukua hatua gani? Na kama wamechukua mbona taarifa hatujaiona wala kuisikia? Kama hawajachukua hatua inamaana na wao pia wanahusika katika hili?
Mimi kama mdau wa Soka hili la Bongo inaniuma sana na kubakia na maswali TFF, FA MIKOA na Benki ya NMB wanatupeleka wapi? Na wapo kwa ajili ya kuendeleza Soka au maslahi yao binafsi? TFF Na Benki ya NMB naomba mchunguze au mtoe maelezo kuhusu hili maana linatia kinyaa na aibu katika Soka letu na kama hamna taarifa basi Habari ndiyo hiyo.
Na Magesa Japhari
E – Mail: japharimagesa@yahoo.com
Mobile phone: +255 784 269 812 or +255 764 318 844, +255 714 368 843.
NB:
Kwa haraka haraka tu, Fedha inayosadikika kutafunwa na TFF na FA MIKOA
Watu 45 @ mkoa × 10,000 gharama ya cheti × 26 mikoa iliyotakiwa kushiriki jumla 11,700,000.
FEDHA ya Wakufunzi mikoa 26,ilitolewa kwa mikoa 10, je mikoa 16@Tshs 710,000 × 16 mikoa ambayo haikutumiwa jumla 11,360,000
GRAND TOTAL Tshs 23,060,000
Hizi ndizo tulizojua kwa mjibu wa hesebu iliyopo je tusizozifahamu ni ngapi? AKILI KUMKICHWA!
UAMUZI WA NEYMAR KWENDA ULAYA - MKUBWA ZAIDI TANGU MESSI ALIPOSAINI BARCELONA KWA KUTUMIA LESO
Lionel Messi alikuwa na miaka 13 tu alipojiunga na Barcelona. Hakukuwa na vita yoyote ya kugombea saini yake, na mkataba wake ulisainiwa kwenye leso haukuwa na shamra shamra nyingi wala kuwasili kwake Nou Camp.
Messi hakuchagua sehemu bora kwake; alikuw na chaguo moja na ndilo alilochagua. Barcelona ndio ilikuwa klabu pekee iliyokuwa tayari kulipa fedha za kumtibu ugonjwa wake wa upungufu wa homoni, na kutokana na imani yao kwa kijana huyu wa Kiargentina leo hii dunia inashuhudia ladha ya soka na klabu inanufaika.
"Nilihitaji fedha kwa ajili ya dawa zangu kunisaidia niweze kukua na Barcelona ilikuwa ndio klabu pekee iliyotoa ofa. Hivyo mara tu walipokubali kunitibia nikajua nitakiwa kuondoka nyumbani na kwenda Catalan," Messi aliliambia jarida la Match of the day. Hiyo ilikuwa mwaka 2000.
Miaka 12 tangu wakati huo kutoka sasa, Messi ameibuka kuwa mchezaji bora kabisa katika kizazi hiki - akiiongoza Barcelona kupata mafanikio makubwa kuliko katika historia ya klabu hiyo, kuanzia nyumbani mpaka ulaya, huku akitajwa mara 3 kuwa mchezaji bora wa dunia (2009,2010, 2011).
Barcelona ingekuwaje bila kuwepo kwa Messi? Unapoangalia takwimu zake za mabao, na mchango wake wote kwa ujumla na namba ya mechi alizocheza kwa kiwango kikubwa na kuipa ushindi Barca, kuna hitimisho moja tu: Wasingekuwa na mafanikio haya au wangekuwa duni kama ilivyokuwa miaka ya 90.
Je wangekuwa wameshinda makombe matano ya La Liga, mawili ya Spanish Super Cup na matatu ya ulaya ambao wameshinda wakati wa uwepo wa Messi?
Ofcourse wasingeweza. Hivyo sio kusema timu za Frank Rijkaard na Pep Guardiola zingetoka mikono mitupu, kwa sababu bila Messi pia walikuwa na timu nzuri kulinganisha na vikosi vya timu nyinginezo barani ulaya. Lakini ni mara ngapi tumeishuhudia Barca ikicheza vizuri bila uwepo wa Messi au akiwa yupo chini ya kiwango?
Ukiangalia nyuma, unaweza kusema uamuzi wa Messi kuondoka nyumbani kwao Argentina na kujiunga Barcelona ndio ulikuwa uamuzi uliobadilisha hatma ya soka la ulaya ndani ya miaka 10 iliyopita.
Ni wazo ambalo linatuleta kwa Neymar - mtu ambaye wengi wanamtaja kuwa Messi mpya ambaye ana machaguo mengi katika timu kubwa za ulaya tofauti na ilivyokuwa kwa Lionel.
Hali ya Neymar ni tofauti sana na ilivyokuwa kwa Messi mwaka 2000. Kijana huyu wa Kibrazil tayari ni jina kubwa sana kwenye soka na tayari ameshaanza kuitawala soka ya dunia.
Ni shujaa wa kuteuliwa pale Santos - akifuata nyayo za Pele - huku akitajwa kuwa ndio mchezaji anayetazamwa kuwa bora zaidi katika miaka 10 ijayo katika ulimwengu wa soka.
Uhamisho kwenda Ulaya ni jambo ambalo linangoja muda tu, kitu ambacho kinaeleza kwanini Neymar amekuwa ndio mchezaji anayeandikwa sana kwenye tetesi za vyombo vya habari katika kipindi cha miaka 3. Kila mtu anajua anaondoka Brazil, lakini ni wachache sana au kuna hakuna anayejua kwa hakika ni lini, ni wapi na jezi ya timu gani atakuwa akivaa huko Ulaya.
Mbrazili mwenzie Dani Alves ni mmoja ya wengi wenye matumaini ataungana na Messi pale Barcelona - dili ambalo mwandishi wa ESPNsoccernet, anaamini limeshafanyika.
Ni kitu cha kusisimua sana kumuona Neymar akiungana Messi, lakini pia kama ilivyo kumuona akiungana na Cristiano Ronaldo pale Real Madrid, Eden Hazard pale darajani Chelsea, Wayne Rooney na Robin van Persie pale Old Trafford au kuungana na David Silva na Sergio Aguero pale Etihad Stadium na Man City.
Timu zote kubwa barani ulaya kwa sasa zimetajwa kuwa zinaweza kumchukua mchezaji huyo, huku gazeti la Metro likiripoti kwamba klabu ya PSG ipo tayari kulipa £85 million mwezi January kumsaini kinda huyo.
Pia kumekuwepo na mawazo kwamba Santos hawatomuuza mchezaji huyo mpaka litakapofanyika kombe la dunia 2014, lakini bei ya Neymar sokoni inapanda, ni vigumu kuamini kwamba wataweza kuimiri na kukataa fedha nyingi katika kipindi cha madirisha matatu makubwa ya usajili yajayo.
Uamuzi wa Neymar kuondoka Brazil - utamaanisha kumpa nafasi kubwa ya mchezaji bora wa kizazi chake kwenye soka. kwa kipaji alichonacho, ana kila kitu cha kumfanya aweze kuitawala soka ya ulaya na kuipeleka timu atakayoichagua katika levo nyingine ya mafanikio - sio tu uwanjani bali pia katika biashara na kuifanya kuwa kubwa zaidi ya ilivyo sasa.
MJADALA: SUAREZ ALIFUNGIWA MECHI 8 KWA UBAGUZI - BARTON MECHI 12 KWA RAFU: JOHN TERRY MECHI 4 KWA UBAGUZI. JE HII NI SAWA???
HAYA NI MAONI YA MCHEZAJI WA JOEY BARTON
"Mechi nne tu? Mwaka mzima wa uchunguzi, siku nne za usikilizwaji wa kesi na adhabu ya kufungiwa mechi 4 tu? Suarez alifungiwa 8.
WAZIRI MKUU WA CAMEROON AINGILIA KATI ISHU YA ETO'O KWENYE TIMU YA TAIFA - AMSHAWISHI ARUDI KIKOSINI
Takribani mwezi mmoja baada ya kuandika barua ya kugoma kuichezea timu ya taifa ya Cameroon, mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa zaidi duniani kwa upande wa soka, Samuel Eto'o sasa anaonekana yupo tayari kwenda kinyume na msimamo wake wa mwanzo na kurudi kuitumikia timu ya taifa lake baada ya kuwa na mazungumzo na waziri mkuu wa nchi hiyo.
Mshambuliaji huyo wa klabu ya Anzhi Makhachkala alifungiwa kwa miezi nane baada ya kuongoza mgomo wa wachezaji dhidi ya Chama cha Soka cha Cameroon kuhusiana na posho zao.
Hata alipomaliza kutumikia adhabu hiyo na kuitwa kikosini, Eto'o alikataa na kusema kwamba hataichezea tena timu ya taifa hadi hapo viongozi wa chama cha soka nchini mwake watakapobadilika na kufanya kazi kwa weledi mkubwa na unaostahili.
Jambo hilo sasa linaelekea kupata ufumbuzi baada ya Waziri Mkuu Philemon Yang kuzungumza yeye mwenyewe na mtupia mabao huyo wa zamani wa Barcelona na kumuomba arudi kikosini ili aisaidie nchi yake inayohaha kupata nafasi ya kufuzu kwa fainali zijazo za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2013).
“Mkuu wa Nchi ameamua kulishughuilikia suala hilo yeye mwenyewe na ametupa maelekezo,” amesema kocha wa Cameroon, Jean-Paul Akono.
“Baadaye tulikutana kuweka mambo sawa na sasa kila kitu kiko vizuri. Hivi sasa yuko tayari, lakini anaweza kukosekana kwa sababu ya majeraha. Tutaendelea kuomba na kusubiri siku za mwisho kabla ya mechi."
Cameroon walichapwa 2-0 katika mechi yao ya ugenini dhidi ya Cape Verde, ambayo ni ya kwanza katika raundi ya mwisho ya kuwania kufuzu kwa fainali za AFCON 2013, na kurejea kwa Eto’o kunatarajiwa kuwaongezea nguvu katika mechi yao ya marudiano mjini Yaounde Oktoba 13.
OFFICIAL: JOHN TERRY AADHIBIWA MECHI NA FAINI YA £220,000 - KUZIKOSA MAN UNITED NA ARSENAL
John Terry ameadhibiwa na chama cha kandanda cha England, FA, asicheze mechi nne, na vile vile alipe faini ya pauni 220,000, kutokana na matamshi ya ubaguzi wa rangi dhidi ya mchezaji wa QPR, Anton Ferdinand.
Chama cha FA kilithibitisha Terry alifanya makosa hayo, baada ya kusikiliza kesi dhidi yake kwa kipindi cha siku nne.
Msemaji wa John Terry alisema mchezaji huyo "alisikitishwa" na hatua ya FA, kwa kuamua tofauti, kinyume na mahakama, ambayo awali ilisema hana makosa.
Mwezi Julai, mahakama ya Westminster mjini London ilipitisha uamuzi kwamba mchezaji huyo, mwenye umri wa miaka 31, hakufanya kosa hilo, la kutumia matamshi ya ubaguzi wa rangi dhidi ya Ferdinand.
Hata hivyo wengi watajiuliza kwa nini adhabu dhidi ya Terry ni nyepesi mno, ikilinganishwa na ile iliyopitishwa dhdi ya mchezaji wa Liverpool, Luis Suarez mwaka jana.
Terry ana muda wa siku 14 kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo, mara tu atakapopokea maelezo ya adhabu hiyo kupitia maandishi.
Adhabu hiyo haitatekelezwa hadi Terry atakapopata nafasi ya kuamua atafanya nini.
Taarifa kutoka klabu yake ya Chelsea iliongezea: "Klabu ya Chelsea inafahamu vyema uamuzi uliopitishwa, na inaheshimu uamuzi huo uliotolewa leo na chama cha FA kumhusu John Terry."
Kutokana na adhabu hiyo John Terry atazikosa mechi nne zilizo chini ya FA, ikiwemo mechi dhidi ya mahasimu wao wa jiji la London Arsenal na Spurs pamoja na Norwich na Manchester United.
Chama cha FA kilithibitisha Terry alifanya makosa hayo, baada ya kusikiliza kesi dhidi yake kwa kipindi cha siku nne.
Msemaji wa John Terry alisema mchezaji huyo "alisikitishwa" na hatua ya FA, kwa kuamua tofauti, kinyume na mahakama, ambayo awali ilisema hana makosa.
Mwezi Julai, mahakama ya Westminster mjini London ilipitisha uamuzi kwamba mchezaji huyo, mwenye umri wa miaka 31, hakufanya kosa hilo, la kutumia matamshi ya ubaguzi wa rangi dhidi ya Ferdinand.
Hata hivyo wengi watajiuliza kwa nini adhabu dhidi ya Terry ni nyepesi mno, ikilinganishwa na ile iliyopitishwa dhdi ya mchezaji wa Liverpool, Luis Suarez mwaka jana.
Terry ana muda wa siku 14 kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo, mara tu atakapopokea maelezo ya adhabu hiyo kupitia maandishi.
Adhabu hiyo haitatekelezwa hadi Terry atakapopata nafasi ya kuamua atafanya nini.
Taarifa kutoka klabu yake ya Chelsea iliongezea: "Klabu ya Chelsea inafahamu vyema uamuzi uliopitishwa, na inaheshimu uamuzi huo uliotolewa leo na chama cha FA kumhusu John Terry."
Kutokana na adhabu hiyo John Terry atazikosa mechi nne zilizo chini ya FA, ikiwemo mechi dhidi ya mahasimu wao wa jiji la London Arsenal na Spurs pamoja na Norwich na Manchester United.
LIGI KUU SUPER WEEKEND KUANZA KESHO
Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom inaingia raundi ya nne kesho (Septemba 28 mwaka huu) kwa mechi za Super Weekend ambazo zitaoneshwa moja kwa moja (live) na kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini.
Mechi ya kwanza ambayo itachezwa kesho itakuwa kati ya Azam na JKT Ruvu Stars. Mechi hiyo itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itaanza saa 1 kamili usiku kwa viingilio vya sh. 3,000 mzunguko, sh. 5,000 kwa VIP C na VIP B wakati VIP A kiingilio kitakuwa sh. 10,000.
Jumamosi (Septemba 29 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Simba na Tanzania Prisons itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni. Yanga na African Lyon zitapambana Jumapili (Septemba 30 mwaka huu kwenye uwanja huo huo kuanzia saa 11 kamili jioni.

















No comments:
Post a Comment