Thursday, October 11, 2012


ADVERTISEMENT

WEDNESDAY, OCTOBER 10, 2012

MIAKA 75 BAADA YA GWIJI LA MANCHESTER UNITED BOBBY CHARLTON KUZALIWA - MFUNGAJI BORA WA MUDA WOTE WA MASHETANI WEKUNDU

Siku kama ya leo miaka 75 iliyopita alizaliwa kiungo mshambuliajimstaafu wa Manchester United na timu ya taifa ya England Sir Bobby Chalton.

Sir Bobby ambaye kwa sasa ni mwanachama wa bodi ya wakurugenzi wa Manchester United ni mmoja kati ya wachezaji wachache walioichezea United mechi nyingi na kufunga mabao mengi, anashika nafasi ya pili nyuma ya Ryan Giggs kwa kucheza mechi nyingi, akiitumikia United katika mechi 758 na kuweza kuifungia mabao 249, akiwa anaongoza katika listi ya wafungaji bora wa muda wote wa klabu ya Manchester United.





Bobby Charlton ni mmoja kati ya wachezaji wanne wa Red Devils ambao wameshawahi kushinda tuzo ya uchezaji bora wa dunia - wa kwanza alikuwa Dennis Law 1964,  akafuatia Charlton 1966, George Best mwaka 1968 na mwaka 2008 Cristiano Ronaldo.
Charlton akiwa na Fergie mwaka 2011

Charlton pia ndio mfungaji bora wa muda wote wa England akiwa ametupia mabao 49 katika mechi 106.

Charlton alikuwa mmoja wa wachezaji waliopata ajali ya ndege wakati United jijini Munich.

Pia siku kama ya leo mwaka mmoja uliopita Shaffih Dauda nilibahatika kupata mtoto wangu wa pili aitwaye Dauda Jr aka Solskjaer ambaye anashea siku moja ya kuzaliwa na mke wangu pia.


Happy Birthday Legend, Happy birthday Wife, Happy Birthday Dauda Jr Solskjaer.


  HII NDIO MAKALA YA VIDEO INAYOELEZEA MAISHA YAKE YA SOKA KIUJUMLA 

GIDABUDAY: WAZIRI USIPOTEZE FEDHA ZA UMMA KUUNDA TUME KWA MADAI AMBAYO USHAHIDI WAKE UPO WAZI

Siku chache baada ya kuwepo kwa taarifa kwamba waziri wa michezo na utamaduni ataunda tume ya kuchunguza TOC, mwanaharakati na mkimbiaji Willlheim Gidabudayi ameibuka na kumuomba waziri asijaribu kuunda tume hiyo kabla kupitia ripoti ya Olimiki kutoka kwa vyama vvya michezo husika kabla ya kuunda tume huru ya kuchunguza TOC kufuatia madai ya ufisadi ambao wadau kama akina Gidabudayi wumetoa sambamba na ushahidi unaoridhisha kama ambavyo ameandika hapo chini:

1). Ni kwa nini waziri asiunde tume ya kuchunguza madai ya DOLA ZA INDIA?, au wizarani pia waliitafuna dola hizo za India?. Dola 100,000 ni takriban TSH: 160,000,000/= ni ajabu sana serikali kudhani kwamba si lolote la kuchunguzwa!!.

2). Pia ni kwa nini hadi leo waziri hajawahoji TOC kuhusu matumizi ya USD 100,000 sawa na TSH: 160,000/= ambazo TOC walidai kuzitumia kwa maandalizi ya kwenda London. TOC walitoa matumizi yao kwa vyombo vya habari lakini matumizi yale yalijaa uongo ambao sisi wadau tunayo ushahidi. Je waziri anadai vipi ripoti ya Olimpiki kabla ya kuchunguza ufisadi ndani ya TOC na baadhi ya maofisa wakubwa wa wizara yake?.

3). Je ni kwa nini hadi leo waziri hajaagiza kupatiwa idadi kamili ya
  fedha zilizotolewa na Olympic Solidarity yaani "quadrennial financial aid" kuanzia 2009 hadi 2012?. Sisi wadau tumeonyesha kutoridhika na kiasi kikubwa kutumiwa na vigogo wa TOC kujinufaisha wenyewe kwa kujijengea mahekalu kana kwamba "wataishi milele".

4). Je watanzania wanafahamu kwamba (Olympic Solidarity inadai kwamba ndio wamelipia gharama za safari ya timu kwenda London!!, pia eti serikali pia ndo waliolipia safari za kwenda London!!). Je watu wenye akili timamu hawapati picha na harufu ya ufisadi?. Je hiyo siyo maana kwamba "hata waziri anapata kigugumizi kuwawajibisha TOC sababu huenda wametafuna wote"?.

MAELEZO MAFUPI KUHUSU NAMBA 4: Inaaminika kwamba (unless they proof otherwise) kuna maofisa kadhaa wizarani pale wenye uwezo wa kuidhinisha fedha, hivyo wanaidhinisha kwamba timu haijalipiwa safari!!, (2004 hadi 2010) wakisha droo hizo hela wanagawana wao na TOC maana safari ilishalipiwa na OS. Pia kuna travel agent moja maarufu jijini Dar (jina nahifadhi) ndo inayotoa risiti feki ili ku - compromise serikalini!!.

5). Je watanzania hawahitaji kujua sababu za mama Pinda kupokonywa
 zawadi ya Olympic Movement na badala yake kupewa mama Bayi, tena aliyempendekeza ni mumewe, je hiyo siyo matumizi mabaya ya madaraka?.
Ukizingatia hata timu ya Olimpiki kukaa kwa Bayi ilikuwa ni Voting Power ya Bayi maana yeye ni (1) Katibu Mkuu TOC, (2). Mjumbe wa RT, (3) Mmiliki wa Hostel zilizotumika kuandaa timu  ya London Games!!.
Kama serikali yetu inahubiri "utawala bora na wa kisheria" inasubiri nini kuunda tume huru kuchunguza madai hayo ili tujue Black or White!!.

MAELEZO MAFUPI KUHUSU NAMBA 5: Olympic Movement ilitaka zawadi apewe mwanamke aliyehamasisha na kuchangia michezo nchini, na jukumu hilo walipewa TOC, inashangaza sana kwamba mama Pinda aliombwa na CHANETA kuchanga fedha ili kufanikisha mashindano ya Africa, tena mama wa watu alijituma na kuonyesha unyenyekevu kwa makampuni makubwa na alifanikiwa kuchangisha mamilioni ya fedha (ambazo matumizi yake hayajawekwa wazi hadi sasa). Lakini katika kilele cha mafanikio
aliyoyasababisha mama yetu mpendwa (TUNU PINDA) zawadi ilikwenda kwa mke wa mtu ambaye (His discretion) ndo ilimuidhinisha mkewe kupata zawadi hiyo kinyemela!!. 

Kumbukeni kwamba Meja Bayi anao uhusiano wa
kimasilahi na CHANETA, pia ana masilahi na MPOKEAJI WA ZAWADI yaani mke wake; Je ni nani basi aliye - play a major roll katika kuamua nani apewe zawadi hiyo kama siyo kamanda mwenyewe!!. "Mimi naamini 100/100 kwamba mke wa waziri mkuu ametumika visivyo na hapo TOC wamedhihirisha
kutokuwa na utu!!. Ndo maana hawastahili hata kupewa haki ya kugombea tena, ndo maana tume huru ya uchunguzi itaweza kupembua UKWELI NA UWONGO.

6). Sasa imefahamika "Mystery behind Puma and Lining". Kumbe PUMA
  ilikuwa inatolewa bure na wadhamini lakini walewale WAIDHINISHAJI wa fedha wizarani (majina tunayo na muda si mrefu tutawataja moja baada ya mwingine), wakawa wana - Bill serikali "kana kwamba Puma hizi hazijalipiwa bado!!, hivyo hela zikitoka zinapigwa mifukoni!!. NDO MAANA SIKU MOJA NIKIWA KTK KIPIMA JOTO LA ITV MHESHIMIWA THADEO ALI BEHAVE KAMA NYOKA ALIYENYANGANYWA PANYA MDOMONI!!, kwani uongo?, watanzania si walishuhudia?. Sasa kama waziri anawaonea haya mafisadi hao mimi nitakwenda hadi Dodoma kuwaomba wabunge wapiganaji kusimamia swala la TUME HURU KUUNDWA DHIDI YA TOC!!, pia tukifikia hatua hiyo majina ya MAFISADI WA WIZARA HUSIKA nitazitaja mbele ya wana jangwani, Msimbazi na wadau wote wa michezo nchini bila kuogopa kuku wala jogoo.

7). Pia wizara na TOC wanatakiwa kuueleza umma iweje wanamichezo waliotuwakilisha London wapate pea moja moja tu ya viatu?. Wakati inaeleweka walistahili kupata begi kubwa lenye vifaa vyote vya michezo sambamba na "memorabilia" zilizowekwa chapa ya 2012 LONDON OLYMPIC GAMES kila mmoja wao. Inaaminika kwamba "kigogo mmoja wa wizara alikwenda London kuwapora wanamichezo mabegi hayo kwa hisani ya TOC ili vifaa hivyo vitumike katika kuwahonga wapiga kura ili BAYI na GULAM warudi madarakani sambamba na timu nzima ya sasa ya TOC ili "mchwa waendelee kutafuta for another 4 yrs".

UDHAMINI WA KAMPUNI YA MIKOPO KUWAKIMBIZA DEMBA BA, CISSE, TIOTE NA BEN ARFA NEWCASTLE??



Kumekuwepo na hisia kwamba Newcastle inaweza kuwapoteza wachezaji wake wenye imani kali ya dini ya kiislamu kama Demba Ba, Papiss Cisse, Cheik Tiote na Hatem Ben Arfa baada ya kusaini mkataba wa udhamini wa jezi ambao unaweza ukawa unakinzana na sheria za dini ya kiislam.

Newcastle wametangaza jana kwamba klabu hiyo imekamilisha dili la mamilioni ya fedha na kampuni ya mikopo ya Wonga, ingawa kumekuwepo na mawazo kwamba Ba, Cisse, Tiote na Ben Arfa wanaweza kukataa kuvaa jezi yenye logo ya kampuni hiyo inayopata faida kutokana na biashara ya kuazima fedha huku wakirudishiwa fedha hizo kwa riba - kitendo ambacho ni kinyume sheria za dini ya kiislamu, kwa maana hiyo wanaweza hata kuondoka ili kuepeukana na dhambi hiyo.

Siku za nyuma mchezaji Freddie Kanoute aligoma kuvaa jezi za Seville zilizokuwa na udhamini wa kampuni ya kamari ya 888.com kifuani. Kanoute mwishowe aliruhusiwa kuvaa jezi siyokuwa na mdhamini lakini akakubali kuvaa jezi yenye logo ya mdhamini wakati wa mazoezi akiwa na maana ya kutoitangaza kampuni hiyo kwa mashabiki wake na waklabu kiujumla.

Swali linabakia je Newcastle watakuwa tayari kuwapoteza wachezaji wao wanne muhimu au watakubalia kuwatengenezea jezi ambazo zitakuwa bila na nembo ya mdhamini mpya? Muda pekee ndio utatoa majibu.

WAYNE ROONEY KUPATA MTOTO WA PILI MWEZI MEI MWAKANI



Coleen Rooney ametangaza kwamba ni mjamzito na anategemea kupata mtoto wa pili.

Mtangazaji wa TV na mumewe, mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney walitangaza kupitia ukurasa wa Twitter kwamba wanatagemea kumuongezea ndugu mtoto wao Kai, ambaye anafikisha miaka mitatu mwezi ujao.

Coleen amasema anategemea kujifungua mwezi May 2013.

Akiandika kwenye ukurasa wake wa Twitter, Coleen alisema: "Watu kadhaa waliotea, hivyo sasa habari zipo nje!! Mimi, Wayne na Kai tuna furaha kwamba tunategemea kupata member mpya katika familia yetu mnamo mwezi May.

"Ni mapema bado lakini tuna furaha kubwa, pia tungependa habari hizizitoke kutoka kwetu sisi kwanza kabla ya mtu yoyote mwingine!"

Baada ya kutangaza habari hizo kwenye Twitter wanandoa hao walipongezwa na watu maarufu mbalimbali wakiwemo marafiki kama Danielle O'Hara, Jude Cisse, Charley Webb na Piers Morgan.

Piers Morgan ambaye ni shabiki mkubwa Arsenal aliandika: "Hongera kwa habari hii nzuri @WayneRooney & @ColeenRoo - na tuombe mtoto apate muonekano wako...."

Rooney na Coleen ambao ni marafiki tangu utotoni walioana nchini Italy mwakak 2008 baada ya kuwa wamechumbiana kwa miaka 5. Walianza mapenzi tangu walipokuwa na miaka 16, wakati Coleen akiwa bado yupo shule.

HAPPY BIRTHDAY: TONY ADAMS

MGOMBEA AGOMA KUHOJIWA NA BABA MKWE WA MPINZANI WAKE.


 



USAILI WA WAGOMBEA MKOA WA MBEYA WATAWALIWA NA VITUKO.

 Na Moses Ng'wat,Mbeya.
 USAILI wa wagombea wanaowania nafasi  mbalimbali  za uongozi  katika chama cha soka mkoa wa Mbeya, (MREFA), jana uligubikwa na vituko vya aina yake,  baada ya mmoja wa wagombea wa nafasi ya Uenyekiti,  kumkataa mjumbe wa kamati ya uchaguzi kwa madai kuwa ana mgongano wa kimasilahi na mpinzani wake.
 Mjumbe wa Kamati ya uchaguzi aliyekataliwa na kulazimika kutolewa ndani ya chumba cha usaili ili haki itendeke kwa mgombea ni Katibu, Prince Mwaihojo, ambaye anadaiwa kuwa ni Mkwe wa mgombea mmoja wa nafasi ya Uenyekiti John Mwamwaja.
 Gazeti hili lilishuhudia katibu huyo wa Kamati ya uchaguzi, akitoka nje muda mfupi tu baada ya mmoja wa wagombea ya nafasi ya uenyekiti Elias Mwanjala, alipoitwa ndani ya chumba cha usaili.
 “Mimi nafikiri lazima nitendewe haki haiwezekani mimi nihojiwe na mtu ambaye anamafungamano ya kidamu na mpinzani wangu, ndio maana nilipofika ndani ya chumba cha usaili nilitoa angalizo na nashukuru Mwenyekiti alielewa na kukubali kumtoa nje ” alisema Mwanjala alipoulizwa.
 Kwa upande wake, Mwaihojo alipoulizwa juu ya sakata hilo la kukataliwa,  alikiri kuwa lilitokea na si la ajabu katika mahala popote ambapo haki inaafutwa, hivyo kitendo hicho hakizuii mchakato wa kuwapata viongozi wa chama hicho.
 Akitoa taarifa ya mchakato wa zoezi hilo baada ya kumalizika, Mwaihojo alisema zoezi hilo la usaili kwa limefanikiwa kwa asilimia 90 kwa kuwa wagombea 14 walifanyiwa usaili na kubakiza wagombea wanne tu ambao watamalizia hawakufanyiwa.
 Kwa mujibu wa Mwaihojo, wagombea wanne ambao hawajafanyiwa usali ni Katibu anayemaliza muda wake Lawrence Mwakitalu, Andongwisye Panja, Thomas Kasombwe Sinkwembe ambao wote walitoa udhulu kutokana na kukabiliwa na shughuli mbalimbali ikiwemo kusimamia mitihani ya kidato cha nne inayoendelea hivi sasa.
 Uchaguzi wa MREFA unatarajia kufanyika oktoba 27, jambo litakalowezesha kupatikana kwa uongozi mpya utakaohudumu kwa miaka mine kama katiba ya chama hicho inavyoeleza.
 Aliwataja watu waliojitokeza kuomba nafasi za uongozi  kwa nafasi ya Mwenyekiti kuwa ni John Mwamwaja ambaye ni makamu Mwenyekiti wa uongozi unaomaliza muda wake, wakati wengine ni Majuto Mbuguyo aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji katika Halmashauri ya
Wilaya ya Tanga, pamoja na Elias Mwanjala ambaye katika uchaguzi Mkuu uliopita aligombea ubunge katika jimbo la Kyela na kuangushwa vibaya na mbunge wa sasa Dk. Harrison Mwakyembe, ambaye pia ni Waziri wa Uchukuzi.
Makamu Mwenyekiti ni  Omary Mahinya, wakati nafasi ya Katibu Mkuu, Lawrence Mwakitalu, anayemaliza muda wake,Suleiman Haroub na Redson Kaisi, ambapo Katibu Msaidizi ni William Mwamlima na nafasi ya Mkutano Mkuu wa Taifa Tahdeo Kalua na Danny Korosso.
Kwa upande mweka Hazina ni Asajile Kavenga, Uswege Luhanga, wakati wajumbe wa kamati ya utendaji ni Lwitiko Mwamndela, Thomas Kasombwe, Boniface Sinkwembe.

STARS INGEKUWAJE ENDAPO VIJANA HAWA WA MAXIMO WANGEKUWEPO HADI SASA?


 Wakati aliyekuwa kocha wa timu ya soka ya Taifa ya Tanzania kwa kipindi cha miaka mine (2006 - 2010), Marcio Maximo alipokuja nchini aliingia na mtazamo tofauti kuhusiana na soka la Tanzania, Maximo aliamini kuwa nchi yoyote amnbayo inahitaji mafanikio ya kweli ya soka ni lazima ijizatiti zaidi katika soka la vijana.

 Hata nchini kwao, Brazil soka la vijana ndiyo msingi wao mkubwa wa mafanikio waliyonao, lakini alitambua kwa nchi changa kama Tanzania si rahisi kuingia haraka katika soka la vijana na kupata mafanikio. Aliamini uchumi na aina yetu ya utekelezaji mambo huwa ni ya taratibu sana, lakini hiyo haikuwa sababu ya yeye kushindwa kuingiza vijana wadogo kutoka katika baadhi ya shule za secondary nchini katika timu ya Taifa kwa nia ya kujifunza kwa manufaa ya siku za usoni ya kikosi hicho.

Wakati wachezaji waliokuwa wakitegemewa na Watanzania kuingia katika matatizo ya kinidhamu, Maximo aliona ni vyema kutembea kila nchi na vijana wadogo kama Jerry Tegete, Kiggy Makassy, Himid Mao Makami, Tumba Sued na wengineo na si wachezaji nyota kama kina Juma Kaseja, Haruna Moshi, Mussa Mgosi, Athuman Idd “Chuji”, Amir Maftah na wengineo ambao kwa mujibu wake walikuwa wavurugaji wakubwa wa program zake za ufundi katika timu hiyo.

Ni miaka takribani sita sasa na ni Himid Mao na Salum Abubakary "Sure Boy" ambao bado wanacheza soka la kiwango cha juu, kuanzia kwa wachezaji vijana walioaminiwa na kupewa thamani kubwa na kocha huyo kama Abdulhalim Humud, Jabir Aziz, Ramadhani Chombo, Salum Telela walioingia katika matatizo ya mara kwa mara ya kinidhamu katika klabu zao, Taifa Stars imeshindwa kusonga zaidi japo vijana hao tayari wameshacheza zaidi ya misimu mitano katika ligi kuu ya Tanzania. Wengi wameshuka viwango na wengine hawapo kabisa katika soka la ushindani.

Wakati Tanzania ikipiga hesabu za kufuzu kwa michuano mikubwa kuanzia mwaka 2006 wengi walitarajia jambo hilo kutokea walau kwa miujiza kutokana na aina ya wachezaji vijana ambao walionesha mwanga wakiwa tayari na uzoefu wa mashindano makubwa ya kiafrika.

JERRY TEGETE; Yeye amekwama kabisa ndani ya timu yake ya Yanga. Kosa kubwa kwake ni pale alipoamua kurudi Tanzania kucheza mechi ‘isiyo na maana’ ya Simba na Yanga, April mwaka 2010, japo alifunga mabapo mawili katika mchezo huo, Jerry aliishia hapo na wala mabao yake hayakuisaidia timu yake kwani walilala 4-3. Amekuwa na miaka miwili migumu katika maisha yake ya soka na kuna wakati alifikiria kuachana na soka, aliingia timu ya Taifa akitokea shule ya Makongo Sekondary mwaka 2006 na mwaka mmoja baadaye akasajiliwa na Yanga ambako yupo hadi sasa. Aliweza kujitambulisha kama mfungaji mahiri zaidi katika soka la Tanzania, kwa kutumia kichwa, kuvizia na daima ni mchezaji ambaye hujipanga vizuri katika nafasi yake, mfungaji wa wafungaji anaendea mwishoni akiwa bado kijana mdogo huku akipigwa benchi mara kadhaa ndani ya Yanga baada ya kukimbia na ofa ya kucheza soka la kulipwa barani ulaya Sweden.
KIGGY MAKASSY KIGGY; Sulley Ally Muntari wa Bongo, alifunga bao kali pale, Cairo miaka mitatu iliyopita huku golini akiwepo kipa bora barani Afrika, Essam El Haidary, Kiggy alifunga bao la umbali wa zaidi ya mita 25 tena akiwa chini ya miaka 22, lilikuwa bao ambalo pengine bado halijafungwa tena katika uwanja wa kimataifa wa Cairo na liliwaaacha watangazaji wa mechi hiyo wakisema ni bao bora kati ya mabao sita ambayo yalifungwa katika mchezo baina ya Misri na Tanzania siku hiyo. Stars ilifungwa mabao 5-1 lakini kuna kitu ambacho kilionesha tulichonacho, vipaji. Mara kadhaa alifunga hivyo katika ardhi ya Tanzania, lakini baada ya misimu miwili ya taabu ndani ya Yanga amekimbilia Simba msimu huu lakini hana makali aliyokuwa nayo kipindi kile.
JUMA JABU; Alipoitwa kwa mara ya kwanza katika timu ya Taifa alikuwa mchezaji wa Ashanti United, alisajiliwa na Simba mwaka 2008 na kudumu hapo kwa miaka minne. Kwa mujibu wa pasipoti yake yupo chini ya miaka 26 lakini Jabu hakuwa na makali kwa kipindi cha miaka miwili ya mwisho akiwa Simba, mara kadhaa alijaribu kuibuka lakini majeraha yakawa yanamrudisha chini. Nahodha wa timu ya Taifa ya vijana ambayo ilifuzu na kuondolewa katika michuano ya Afrika mwaka 2005 kwa kudanganya umri kwa kiungo Nurdin Bakary, amekimbilia timu ya Coastal Union ya Tanga na anafanya vizuri kiasi tofati na alipokuwa Simba, akicheza namba sita Jabu alijitambulisha kama mpigaji mzuri wa mipira ya ‘free kick’ na mipira ya penati na kona. Alikutana na kipindi kigumu cha maumivu akiwa Simba na inawezekana ikiwa sababu kubwa ya yeye kuanguka kisoka akiwa bado kijana.

TUMBA SUED; Kuna wakati, Azam FC ilikuwa na wachezaji watu ndugu katika kikosi chao cha kwanza, Tumba Sued alikuwa ni beki mzuri wa kati ambaye alikuwa anaitwa mara kwa mara katika timu ya Taifa kwa nia ya kuendelezwa alikuwa akitokea timu ya vijana ya Azam na haraka akawa ‘patna’ mzuri na kaka yake Salum Sued katika ngome ya kati ya Azam, wakati Said Sued akifanya vizuri katika nafasi ya kiungo, Tumba akatokea kuwa beki bora kijana nchini mbele ya majeruhi Dickson Daudi, haraka alipopata mafanikio katika msimu wake wa kwanza akiicheza timu kubwa ya Azam, Tumba akiingia katika maisha ya ndoa na mara kadhaa akaingia katika matatizo ya kinidhamu na klabu yake na hata alipoenda timu ya Moro United hakuwa yule ambaye alitajwa mara kwa mara na kocha, Maximo katika kikosi chake kwa nia ya kuja kuisadia timu hiyo katika siku za usoni, amepotea na wala hasikiki tena.

DICKSON DAUD; Rafu mbaya ambayo alichezewa na mmoja wa wachezaji wa timu ya JKT Ruvu katika mchezo wa ligi kuu ndogo kituo cha Dodoma mwaka 2007, inawezekana kabisa ndiyo iliyommaliza, wakati Maximo akitamba na ukuta wa nidhamu wa Victor Costa, Salum Sued, Hamis Yusuph na Nadir Haroub hakuwa na mashaka na warithi wa nafasi zao hata kama kungetokea majeraha yoyote, Dickson Daud alikuwa beki bora zaidi wa kati U23 katika miaka ya mwanzo ya kocha maximo alikuwa mlinzi shupavu na aliyekuwa na uwezo mkubwa wa kuruka juu na kufunga mabao ya vichwa, anahitaji kujiamini tena kama anataka kuwa mchezaji mzuri tena, ameanza vizuri msimu huu na tayari ameonesha mwanga mkubwa kuwa ataibuka tena, alifunga bao zuri katika mechi ambayo timu yake ya Mtibwa iliifunga Yanga mabao 3-0.

SALUM KANONI; Huyu alichukuliwa kama mbadala wa muda mrefu wa beki namba mbili wa Stars, Shadrack Nsajigwa, lakini mara baada ya kujiunga na Simba mwaka 2005 akitokea Bandari ya Mtwara, Kanoni akawa namba mbili mbadala wa walinzi Said Sued na Nurdin Bakary walipokuwa na majeraha, lakini hata pale nyota hao walipokuwa wazima ilibidi wapambane kugombea nafasi ya kucheza mbele ya kinda huyu, taratibu akachukua nafasi ya kudumu ndani ya Simba na kuitwa Stars na kucheza baadhi ya michezo chini ya makocha, Maximo na hata wakati wa Jan Poulsen, Tatizo lake kubwa ni kuridhika na kujiona tayari amefika safari yake ya soka ndani ya Simba, na baada ya miaka saba, akiwa ndani ya klabu hiy, Kanoni ameondolewa na sasa yupo Kagera Sugar akijaribu kupigania kurudisha makali yake, ameshafunga mabao mawili katika ligi kuu hadi sasa, so far anaendelea vizuri. 

ABDULHALIM HUMUD; Gaucho wa Tanzania, alikuwa ni kiungo ‘maestro’ ambaye aliweza vyema jukumu la kushambulia na kuzuia ‘box to box’ aliyekuwa na uwezo na mapafu yasiyochoka, tabia mbaya na kujiona ni mkali zaidi ya hata, Mohammed Aboutrika, Ricardo Kaka’, Alex Song na hata Yaya Toure vimemmaliza alitua Simba na kushindwa kuchomoza mbele ya wachapa kazi kama Jery Santo na Hillary Echessa na kukimbia benchi, akaenda Azam lakini tayari ameonekana kuzidiwa nguvu na Ibrahimu mwaipopo katika kiungo wa ulinzi ndani ya Azam na wakati vijana Himid Mao na Salum Abubakary wakihitaji mafanikio ya mchezo wao Humud anapigana kurudisha makali yake chini ya kocha Boris Bunjuk ambaye ameonekana kumuamini kiungo huyu.

KOCHA WA YANGA TOM SAINTFIET APATA KAZI YA UKOCHA NCHINI YEMEN


Siku chache baada ya kufutwa kazi ya kuiongoza timu ya Young Africans ya nchini Tanzania, Kocha Tom Saintfiet raia wa Ubelgiji amepata ajira mpya ya kukinoa kikosi cha timu ya taifa ya Yemen.

Tom alifutwa kazi na timu ya Yanga baada ya timu hiyo kuanza vibaya katika michuano ya ligi kuu ya Vodacom licha ya kuisaidia kutwaa taji la mashindano ya kanda ya Afrika Mashariki na Kati.

Saintfiet, ambaye aliwahi kuwa kocha wa Ethiopia ameanza kazi siku ya Jumamosi na ataiongoza timu yake mpya dhidi ya Lebanon katika mechi ya kirafiki iliyopangwa kufanyika Oktoba 16.

TENGA AZITAKA KAMATI ZA UCHAGUZI KUSIMAMIA KANUNI



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amezitaka Kamati za Uchaguzi kufanya kazi kwa kuzingatia Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF ili kuwa na uchaguzi huru na wa haki. Akizungumza na Waandishi wa Habari, Dar es Salaam leo, Rais Tenga amesema uongozi wa mpira wa miguu unahitaji uamuzi mgumu, hivyo Kamati za Uchaguzi ambazo zimeundwa kwa mujibu wa Katiba zinatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni na si kuangalia sura za watu.

Amepongeza kamati zilizosimamia uchaguzi kwa kufuata kanuni, na ingawa kila mtu ana haki ya kuongoza, jambo lolote lazima liwe na kanuni, kwani hata kwenye mikutano ya hadhara kuna kanuni. “Huwezi kufika kwenye mkutano wa hadhara na wewe unaanzisha mkutano wako. Lazima kanuni ziheshimiwe ili kufanya uchaguzi uwe huru na wa haki. Nini kimetokea kwenye maeneo ambayo kuna matatizo? Kila mwanachama wetu (mkoa/chama shiriki) ana Kamati ya Uchaguzi ambayo imeundwa kwa mujibu wa kanuni.

 “Zile kamati hazitekelezi majukumu yake, unampitisha mtu unajua hana sifa unasema acha akafie mbele (Kamati ya Uchaguzi ya TFF). Kanuni zinasema jaza fomu mwenyewe, weka nakala za vyeti na si kwamba huyu tunamjua. Kanuni zinatakiwa zifuatwe, ukienda kinyume unaondolewa,” amesema. Amesisitiza kamati zifanye kazi kwa kufuata kanuni ili kusaidia mpira wa miguu kwani zimeundwa kihalali, kwa hiyo zisiogope kuengua hata walioziteua kama hawana sifa. Pia Rais Tenga amezitaka Kamati za Utendaji na Sekretarieti kutoziingilia Kamati za Uchaguzi katika mchakato wa uchaguzi, badala yake zinatakiwa kuziwezesha tu (facilitation).

Amesema baadhi ya wagombea nao ni tatizo kwani wanaingia kwenye uchaguzi bila kuzielewa Katiba za vyama vyao na Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF, hivyo ni vizuri wakazielewa kwanza. Rais Tenga amesema ni vizuri wanachama wote wakafanya uchaguzi kabla ya uchaguzi wa TFF utakaofanyika Desemba mwaka huu ili wapate fursa ya kupiga kura kwenye uchaguzi huo wa shirikisho. Vilevile amewataka wadau kujitokeza kwa wingi kuwania uongozi kwenye chaguzi za vyama wanachama wa TFF, kwani mwitikio umeonekana kuwa mdogo kulinganisha na umaarufu wa mchezo wenyewe. Amepongeza vyama vya mikoa ambavyo tayari vimefanya uchaguzi wao. Baadhi ya vyama hivyo ni Arusha, Dodoma, Iringa, Kagera, Kigoma, Kilimanjaro, Manyara, Mara, Morogoro, Mtwara na Singida. Boniface Wambura Ofisa Habari Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

HUU NI UZALENDO ATOA KALI NYINGINE! AMWAGA CHOZI BAADA YA YANGA KUTOKA SARE NA SIMBA.

TUESDAY, OCTOBER 9, 2012

GOLI BORA LA SIKU - JESUS MARTINEZ

MCHEZAJI WA AC MILAN AWA WAZIRI MKUU MSAIDIZI NA WAZIRI WA MIUNDOMBINU NCHINI GEORGIA



Mchezaji wa zamani wa AC Milan Kakha Kaladze amethibitishwa kuwa waziri mkuu msaidizi wa nchi ya Georgia.

Mshindi wa mara mbili wa UEFA Champions league  akiwa na Milan, Kaladze amekuwa makamu wa waziri mkuu na pia waziri wa miundo mbinu na maendeleo katika serikali mpya ya Georgia.

Kakha Kaladze baada ya kuwa mwanasiasa
"Nilipotangaza kustaafu kucheza soka, nilisema mechi muhimu zaidi ya maisha yangu ndio imeanza sasa," alisema mlinzi huyo mstaafu mwenye miaka 34 akiongea na shirika la habari la AFP wakati wa kampeni za uchaguzi.

Kampeni za uchaguzi zilizianza kuwa chafu baada ya kituo cha TV cha serikali utoa mikanda ya video ambayo walisema inatoa ushahidi kwamba baadhi wanasiasa, akiwemo Kaladze walikuwa na mahusiano mabosi makundi yanayofanya vitendo vya makosa  - tuhuma ambazo Kaladze aliziita za kijinga. 

“Sina chochote kinachohusiana na Mafia, sio mwanzoni huko nyuma wala sasa," anasema Kaladze.
"Mip[ango yangu kwa sasa ni kutengeneza vizuri barabara na kutoa huduma nzuri za usambazaji wa maji."

AKINA OZIL, GOMEZ NA PODOLSKI WAAHIDIWA €20,000 KWA KILA MECHI MPAKA WATAKAPOFUZU KUCHEZA WORLD CUP 2014

Wachezaji wa timu ya taifa ya Ujerumani watapokea kiasi cha €20,000 kwa kila mechi ya kufuzu kombe la dunia watakayocheza na ikiwa watafanikiwa kufika nchini Brazil 2014, chama cha soka cha hiyo DFB kimethibitisha.

Kila mchezaji atapata kiasi hicho chote cha fedha kwa kila mechi ya kufuzu, lakini watapokea kiasi hicho mara watakapoweza kufuzu kwenda kwenye michuano ya hiyo ya dunia itakayofanyika nchini Brazil 2014.

"Nina furaha na uharaka na kutokuwepo kwa matatizo katika makubaliano haya. Hii inaonyesha uaminifu uliopo kati ya shirikisho na wachezaji wa timu ya wakubwa ya soka ya Ujerumani," alisema Raisi wa shirikisho hilo Mr.Wolfgang Niersbach.

Ujerumani tayari wameshashinda mechi zao mbili za kundi C na mpaka sasa wanapewa nafasi kubwa ya kuwa viongozi wa kundi hilo  kwa kuongeza pointi 6 nyingine watakapocheza na Irealnd na Sweden Ijuma na Jumanne ijayo.
 

MTOTO WA MANUTE BOL KATIKA HARAKATI ZA KURITHI UWEZO WA BABA YAKE KATIKA NBA

ENGLAND WAZINDUA KITUO CHA ST.GEORGE PARK CHENYE THAMANI YA £100 MILLION


Mjukuu wa Malkia wa Uingereza Prince William na mkewe Kate wakizindua kituo cha St.George Park





Frank Lampard akitaniana na Duchess of Cambridge - mke wa Prince William ambaye ni Raisi wa FA.

Raisi wa FA Prince William akizungumza na wachezaji wa England

Game for a laugh: Wayne Rooney jokes with England coach Gary Neville
Wayne Rooney akifurahia jambo na kocha wake msaidizi Gary Neville

Prince William akimtania Ashley Cole - Mchezaji ambaye juzi aliwatolea maneno machafu chama cha soka cha FA ambacho mjukuu huyo wa Malkia ndio Raisi.

Wachezaji wa England wakiwa kwenye Jaccuzi wakipumzika baada ya mazoezi

Kituo cha ST.George Park kilivyo

St.George Park

Hostel za kituo cha St.George Park

Uwanja wa ndani wa soka uliopo ndani ya kituo cha St.George Park

KWA USHAHIDI HUU NI KWELI LUIS SUAREZ ANAONEWA AU ANAJIRUSHA KWELI??


BAADA YA MASHABIKI KUGOMA KUINGIA UWANJANI - WACHEZAJI WA DINAMO WATOA MKWANJA MREFU KUWASHAWISHI MASHABIKI KUJAA UWANJANI

Baada ya kuumizwa na kitendo cha kucheza mechi za Champions league katika uwanja uliokaribia kuwa mtupu, wachezaji wa Dinamo Zagreb wameamua kuchanga fedha kwa ajili ya kuchezesha bahati nasibu ili kuwavutia mashabiki kuingia katika mechi yao ya Champions league inayofuatia dhidi ya PSG. Dinamo walicheza mechi yao iliyopita uwanjani kukiwa na watu wasiozidi 15,000 katika uwanja wenye siti zaidi ya 38,000, katika mechi dhidi ya Porto. Mashabiki wa klabu hiyo wamekuwa wakiachana na kwenda kwenye mechi wakiwekea mgomo bei za tiketi na kuonyesha kutokubalina na uongozi wa klabu hiyo. Hivyo ili kushawishi mashabiki, wachezaji wa timu hiyo wameamua kutoa ofa ya million moja za kunas ambazo ni sawa na $174,000 katika bahati nasibu kwa wanunuzi wa tiketi wa mechi zao.

Kutoka AFP:
Wazo hilo lilianzishwa na kiungo Mateo Kovac ambaye aliweka video, "Million moja kwa uwanja ukijaa" katika ukurasa wake wa faceboo, kwenye viedo iliyokuwa ikimuonyesha akiongea na wachezaji wenzie. 
Katika press conference ya Ijumaa iliyopita wachezaji walisema kiwango cha zawadi ya fedha kitategemeana na namba ya mashabiki watakaoingia kwenye uwanja katika mechi yo dhidi ya PSG itakayofanyika mwezi huu tarehe 24.
Million moja ya kunas otatolewa ikiwa tu zaidi ya mashabiki 25000 watakuja uwanjani.


ADAM MATUNGA: MAXIMO ALINISHAURI NISIJIUNGE NA YANGA - ATALIA AKIRUDI NCHINI NA KUNIONA




Kwa mchezaji ambaye amezaliwa mwaka 1989 bila shaka bado ni angali kijana hasa ambaye anaweza kutimiza ndoto zake za kimaisha kwa kutumia kipaji chochote ambacho hutokea kujaliwa na mwenyezi Mungu.

 Adam Matunga ni mchezaji wa mpira wa miguuu, na ni kijana ambaye amejaliwa kipaji cha hali ya juu cha mchezo huu, hasa akicheza kama kiungo mshambuliaji, aliwahi mara kadhaa kuitwa na kuitumikia timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars chini ya kocha wa Kibrazil, Marcio Maximo. Alikuwa ni mmoja wa vijana wa mwanzo kuingizwa timu ya Taifa kwa nia ya kuendelezwa ili waje waisaidie timu hiyo katika siku za usoni, aliingia hasa katika moyo wa kocha, Maximo na bahati kubwa kwake ni kwamba aliitwa akitokea timu ya moani ya AFC Arusha mwaka 2007. Lakini yupo wapi hivi sasa, ana fanya nini na kwa nini hasisiki tena kama matarajio ya wengi yalivyokuwa yakifikiria? 

Yote haya www.shaffihdauda.com inakuletea baada ya kumkuta kijana huyu wa mwaka 1989 akicheza soka la‘Kiveterani’ na wakongwe kina Sanifu Lazaro ‘Tingisha’ na Sekilojo Johnson Chambua…..

SWALI; Mbona kimya na hausikiki tena katika soka la Tanzania, nini kimekusibu?

MATUNGA; Nilipata matatizo makubwa ya goti nikiwa Mtibwa Sugar mwaka 2008, na kuna wakati nikapatwa na hisia mbaya kuhusiana na mchezo huu, sikuona faida yake kwani viongozi wengi ni waongo, unakaa kambini kwa miezi mingi unarudi nyumbani hata pesa ya likizo hapewi. Nadhani ni wachezaji wachache sana ndiyo wanaofaidika na soka la nchi hii. Ukitazama hata hao waliopo timu kubwa wengi wana maisha mabovu sana Kaka , hilo nalo lilinikatisha sana tamaa. Unajua kuna wachezaji wapo Simba na Yanga wanawaomba wale ambao wapo mitaani msaada, kweli inatakiwa moyo kucheza mpira katika nchi hii.

SWALI; Je, hiyo ndiyo unadhani sababu kubwa ya wewe kukufanya ushindwe kutimiza malengo yako?

MATUNGA; Mimi bado kijana mdogo na bado nina ndoto za kufanikiwa katika soka, lakinmi niliamua kupumzika kidogo ili nitafute kwanza pesa ili nije niucheze pasipo kuwa na mawazo, na hata hilo la ‘usanjo’ wa viongozi wengi wa mpira nchini unachangia kuwaondoa vijana wengi kwenye soka. Mimi najiandaa kurejea uwanjani kwani hivi sasa nitacheza soka bila kuwa na mawazo kwani nilichokuwa nakitafuta ( pesa) nimeshapata.

SWALI; Ipi ni timu yako ya mwisho kuichezea na Je, kwa upande wa kambi ya timu ya Taifa kwa kipindi kifupi ambacho wewe ulikuwa katika kikosi hicho ulikutana na hali hii ya ‘usamjo’ wa viongozi hasa katika masuala ya ulipaji wa posho?

MATUNGA; Manyema Rangers ndiyo timu yangu ya mwisho kuicheza kabla sijaamua kutafuta pesa kwanza, ilikuwa ni mwaka 2010. Kwa upande wa timu ya Taifa kama kulikuwa na matatizo nadhani ni miaka ya nyuma, kwa muda ambao mimi nilibahatika kuingia kikosini sikuona hali hiyo, posho ilikuwa inakuja kwa wakati na ilikuwa imepanda pia, timu ilikuwa inafilkia na kuweka kambi katika hotel kubwa na zenye hadhi. Nadhani yote hii sababu ya kocha, Maximo yeye alikuwa ni zaidi ya kocha, alikuwa ni kama Baba kwa wachezaji wengi nchini, ndiye aliyebadilisha maisha ya wachezaji wengi nchini ‘ per day’ ilikuwa nzuri, mnalala sehemu nzuri , binafsi ninamkubali sana Maximo na kanisaidia sana Kaka.

SWALI; Unamzungumziaje, Maximo na vitu gani ambavyo alikuwa akikwambia kama msaada wako katika siku za usoni?

MATUNGA; Ukweli ni vitu vingi sana ambavyo aliniambia na ndiyo ambavyo nimekuwa nikivitumia hasi leo katika maisha yangu, kama nilivyokwambia awali kuwa Maximo alikuwa zaidi ya kocha hivyo alijua maisha ya wachezaji wa Kitanzania yalivyo hivyo alikuwa akinambia hata mambo ya kufanya kama binadamu ninayehitaji kuwa na maisha mazuri. Kikubwa nachokumbuka aliniambia ‘ Usiichague Yanga, nenda Mtibwa kwa manufaa ya mchezo wako” hakutaka mimi niende Yanga kwa sababu alioniona bado kijana mdogo na nisingeweza kuhimili presha ya timu hiyo, hivyo akaniambia niende Mtibwa na kweli nikafanya hivyo. 

SWALI; Unadhani kwa nini alikwambia usiende Yanga na uende Mtibwa wakati wengi huchagua kwanza Yanga ama Simba na si timu za mikoani pale wanapopata ‘ofa’ kama yako?

MATUNGA; Aliniambia nikicheza Mtibwa nitakuwa na kiwango kizuri zaidi kwani nilikuwa bado mdogo na alihitaji kuniona nikikua taratibu, pia aliniambia presha iliyopo Mtibwa ni ndogo tofauti na iliyopo Yanga hivyo kwa umri wangu mahala sahihi aliona ni kule, na kweli nilifurahi sana nilipokuwa katika klabu ile ( Mtibwa)
SWALI; Unadhani, Maximo akija Tanzania hivi sasa na kukuona ukicheza mechi za ‘veterani’ atajisikiaje, kwani alikuwa na matarajio makubwa kukuona ukipata mafaniko katika soka?

MATUNGA; Atasikitika sana kaka. Yaani alikuwa akiniona ni bonge la mchezaji kila nilipokuwa uwanjani, alikuwa anapenda kunitazama, na mara zote alihitaji kuona wachjezaji wenzangu wananipasia mipira mimi. Utamsikia nje akisema “ ADAM, VOMELAA VOMELAA ( Adam zungushaa, zungusha), alikuwa akiniambia nacheza soka la kibrazil, furaha yake ilikuwa kuniona mimi namiliki mpira.

SWALI; Mara ngapi uliiwakilisha Stars chini yake (Maximo) na nini malengo yako sasa?

Chini ya Maximo mara tatu niliichezea Stars na pia nilipata kuicheza Kilimanjaro Srars ( Tanzania Bara). Narudi uwanjani kumuenzi marehemu, Baba yangu ambaye alikuwa akihitaji kuniona mwanae nacheza tena soka , nilimpenda sana Baba yangu lakini mungu amempenda zaidi, narudi uwanjani kwa nguvu zote sina mawazo ya pesa tena itakuwa ni soka tu kwani ndiyo furaha yangu.
SWALI; Unadhani nini kinachangia ugumu wa maisha kwa wachezaji wengi wa ligi kuu nchini?

MATUNGA; Malipo ni madogo sana na maisha yanapanda kila siku, mchezaji huwezi kupata mafanikio kama unaishi maisha ya kubahatisha ni lazima ule vizuri na hata wachezaji wanakimbilia kusaini hovyo mikataba wakati ukweli wa maisha ni tofauti na wanachosaini wachezaji ambao wanapata bahati ya kushika walau vimillioni ni vyema wakakumbuka kuwa kuna maisha nje ya soka, wapunguze kuishi Ki-star waukubali ukweli na wafungue miradi ambayo itawasitiri mara baada ya kumaliza kucheza soka. Pia ni wakati pia kwa viongozi kuwathamini na kuwajali wachezaji, wasiwacheweleshee mishahara yao na watazame pia hata malipo yao ya posho na aina ya maisha ya sasa. 

SWALI; Umekuwa ukijumuika na kucheza pamoja na wachezaji ‘veterani’ kina Sekilojo Chambua na Sanifu Lazaro ambao kimsingi tayari wameshashinda mataji makubwa hapa nchini, kitu gani wamekuwa wakikueleza na ambacho kinawauma kukuona ukijumuika nao wao badala ya kuwa miongoni mwa wachezaji wa timu ya Taifa?

Wamekuwa waninisisitiza umuhimu wa mimi kurejea uwanjani na kucheza soka la ushindani, kila napokutana na wao hayo maneno lazima waniambie na sitawangusha najiaanda., inshalah Mungu akijalia ‘next season’ nitakuwa uwanjani tena 

SWALI; Unacheza kama nani?

MATUNGA; Kama Iniesta Kaka nampenda sana Iniesta anaisadia sana timu yake ya Barcelona na ie ya Hispania 

SHABIKI WA YANGA AFARIKI BAADA YA KUSHINDA KWENYE SHINDANO LA KULA MENDE MAREKANI


Edward akila mende
Mshindi wa shindano la kula mende amefariki dunia muda mfupi  kula mende wazima huko Florida -Marekani, polisi wamesema.

Edward Archbold, 32, ambaye alisema kwamba ameshawahi kula wadudu hao huko nyumbani kwao Dar es Salaam, Tanzania alianza kuumwa na hatimaye kuanguka katika duka la wadudu mahala ambapo shindano hilo lilikuwa likifanyika katika mji wa Deerfield Beach Ijumaa iliyopita.

Kuna zaidi ya watu 30 walioshiriki shindano hilo katika duka la Ben Siegel Reptile Store.
Mamalka zinasubiri matokeo ya vipimo vya hosptali ili kujua chanzo cha kifo cha Archbold.

Hakuna mtu yoyote aliyeshiriki kwenye shindano hilo aliyeumwa baada ya kumalizika kwa shindano hilo, walisema polisi.
"Tumesikitika sana juu ya tukio hili," alisema Ben Siegel , mmiliki wa duka la wadudu.
""Alionekana kama alitaka kujionyesha na alikuwa mtu mzuri sana," alisema, akiongeza kwamba Archbold hakuonekana kuwa anaumwa kabisa.

Mwanasheria wa Mr.Siegel  alisema kwamba washiriki wote walisaini maelezo kwamba "wanakubaliana na matokeo yoyote yatakayotokea kutokana na kushiriki mchezo huo wa ajabu.

Mr.Archbold ambaye alikuwa anajulikana kwa mapenzi yake makubwa kwa timu ya Young Africans ya nchini Tanzania, alishinda shindano hilo lakini badae kidogo akadondoka na kufa

No comments:

Post a Comment